< Zaburi 146 >

1 Msifu Yahwe. Msifu Yahwe, ee nafsi yangu.
Alléluiah. Psaume d'Aggée et de Zacharie. Ô mon âme, loue le Seigneur;
2 Ninamsifu Mungu maisha yangu yote; nitamuimbia sifa Mungu wangu ni ngali ni hai.
Je louerai le Seigneur toute ma vie; je chanterai des psaumes à mon Dieu tant que j'existerai. Ne mettez point votre confiance dans les princes,
3 Msiweke imani katika wakuu au wanadamu, ambaye katika yeye hamna wokovu.
Ni dans les fils des hommes; car ils n'ont point de salut.
4 Wakati uhai wa pumzi ya mtu unapokoma, hurudi aridhini; siku hiyo mipango yake hufikia mwisho.
Leur esprit s'évanouira, et ils retourneront en leur terre; en ce jour- là périront toutes leurs pensées.
5 Amebarikiwa yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yahwe Mungu wake.
Heureux celui qui a pour champion le Dieu de Jacob, son espérance dans le Seigneur son Dieu,
6 Yahwe aliumba mbingu na nchi, bahari, na vyote vilivyomo; huitazama kweli milele.
Qui a créé le ciel et la terre, et la mer, et tout ce qu'ils renferment;
7 Yeye hutekeleza hukumu kwa ajili ya walioonewa na huwapa chakula wenye njaa. Yahwe huwafungua waliofungwa;
Qui garde la vérité dans tous les siècles, qui rend justice aux opprimés; qui donne aux pauvres la nourriture. Le Seigneur délivre ceux qui sont enchaînés.
8 Yahwe huyafungua macho ya kipofu; Yahwe huwainua walioinama; Yahwe huwapenda watu wenye haki.
Le Seigneur rend sages les aveugles; le Seigneur relève ceux qui sont brisés; le Seigneur aime les justes.
9 Yahwe huwalinda wageni katika nchi; huwainua yatima na wajane, bali huipinga njia ya wasio haki.
Le Seigneur garde les étrangers; il secourt l'orphelin et la veuve, et il exterminera la voie des pécheurs.
10 Yahwe atatawala milele, Mungu wako, Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Yahwe.
Le Seigneur ton Dieu, ô Sion, régnera dans tous les siècles, de génération en génération.

< Zaburi 146 >