< Zaburi 146 >
1 Msifu Yahwe. Msifu Yahwe, ee nafsi yangu.
Louez Yah! Loue Yahvé, mon âme.
2 Ninamsifu Mungu maisha yangu yote; nitamuimbia sifa Mungu wangu ni ngali ni hai.
Tant que je vivrai, je louerai Yahvé. Je chanterai les louanges de mon Dieu aussi longtemps que j'existerai.
3 Msiweke imani katika wakuu au wanadamu, ambaye katika yeye hamna wokovu.
Ne mettez pas votre confiance dans les princes, dans un fils d'homme en qui il n'y a pas de secours.
4 Wakati uhai wa pumzi ya mtu unapokoma, hurudi aridhini; siku hiyo mipango yake hufikia mwisho.
Son esprit s'en va, et il retourne à la terre. En ce jour même, ses pensées périssent.
5 Amebarikiwa yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yahwe Mungu wake.
Heureux celui qui a pour secours le Dieu de Jacob! dont l'espoir est en Yahvé, son Dieu,
6 Yahwe aliumba mbingu na nchi, bahari, na vyote vilivyomo; huitazama kweli milele.
qui a fait le ciel et la terre, la mer, et tout ce qui s'y trouve; qui garde la vérité pour toujours;
7 Yeye hutekeleza hukumu kwa ajili ya walioonewa na huwapa chakula wenye njaa. Yahwe huwafungua waliofungwa;
qui exécute la justice pour les opprimés; qui donne de la nourriture aux affamés. Yahvé libère les prisonniers.
8 Yahwe huyafungua macho ya kipofu; Yahwe huwainua walioinama; Yahwe huwapenda watu wenye haki.
Yahvé ouvre les yeux des aveugles. Yahvé relève ceux qui sont courbés. Yahvé aime les justes.
9 Yahwe huwalinda wageni katika nchi; huwainua yatima na wajane, bali huipinga njia ya wasio haki.
Yahvé préserve les étrangers. Il soutient l'orphelin et la veuve, mais il renverse la voie des méchants.
10 Yahwe atatawala milele, Mungu wako, Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Yahwe.
Yahvé régnera à jamais; ton Dieu, Sion, de génération en génération. Louez Yah!