< Zaburi 146 >
1 Msifu Yahwe. Msifu Yahwe, ee nafsi yangu.
Praise ye the LORD! Praise the LORD, O my soul!
2 Ninamsifu Mungu maisha yangu yote; nitamuimbia sifa Mungu wangu ni ngali ni hai.
I will praise the LORD, as long as I live; I will sing praises to my God, while I have my being.
3 Msiweke imani katika wakuu au wanadamu, ambaye katika yeye hamna wokovu.
Put not your trust in princes, In the son of man, in whom is no help!
4 Wakati uhai wa pumzi ya mtu unapokoma, hurudi aridhini; siku hiyo mipango yake hufikia mwisho.
His breath goeth forth; he returneth to the dust; In that very day his plans perish.
5 Amebarikiwa yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yahwe Mungu wake.
Happy is he that hath the God of Jacob for his help; Whose hope is in the LORD, his God;
6 Yahwe aliumba mbingu na nchi, bahari, na vyote vilivyomo; huitazama kweli milele.
Who made heaven and earth, The sea, and all that is therein; Who keepeth truth for ever;
7 Yeye hutekeleza hukumu kwa ajili ya walioonewa na huwapa chakula wenye njaa. Yahwe huwafungua waliofungwa;
Who executeth judgment for the oppressed; Who giveth food to the hungry. The LORD setteth free the prisoners;
8 Yahwe huyafungua macho ya kipofu; Yahwe huwainua walioinama; Yahwe huwapenda watu wenye haki.
The LORD openeth the eyes of the blind; The LORD raiseth up them that are bowed down; The LORD loveth the righteous.
9 Yahwe huwalinda wageni katika nchi; huwainua yatima na wajane, bali huipinga njia ya wasio haki.
The LORD preserveth the strangers; He relieveth the fatherless and the widow; But the way of the wicked he maketh crooked.
10 Yahwe atatawala milele, Mungu wako, Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Yahwe.
The LORD shall reign for ever; Thy God, O Zion! to all generations! Praise ye the LORD!