< Zaburi 146 >
1 Msifu Yahwe. Msifu Yahwe, ee nafsi yangu.
Praise ye the Lord. Praise thou the Lord, O my soule.
2 Ninamsifu Mungu maisha yangu yote; nitamuimbia sifa Mungu wangu ni ngali ni hai.
I will prayse the Lord during my life: as long as I haue any being, I wil sing vnto my God.
3 Msiweke imani katika wakuu au wanadamu, ambaye katika yeye hamna wokovu.
Put not your trust in princes, nor in the sonne of man, for there is none helpe in him.
4 Wakati uhai wa pumzi ya mtu unapokoma, hurudi aridhini; siku hiyo mipango yake hufikia mwisho.
His breath departeth, and he returneth to his earth: then his thoughtes perish.
5 Amebarikiwa yule ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake, ambaye tumaini lake liko katika Yahwe Mungu wake.
Blessed is he, that hath the God of Iaakob for his helpe, whose hope is in the Lord his God.
6 Yahwe aliumba mbingu na nchi, bahari, na vyote vilivyomo; huitazama kweli milele.
Which made heauen and earth, the sea, and all that therein is: which keepeth his fidelitie for euer:
7 Yeye hutekeleza hukumu kwa ajili ya walioonewa na huwapa chakula wenye njaa. Yahwe huwafungua waliofungwa;
Which executeth iustice for the oppressed: which giueth bread to the hungry: the Lord loseth the prisoners.
8 Yahwe huyafungua macho ya kipofu; Yahwe huwainua walioinama; Yahwe huwapenda watu wenye haki.
The Lord giueth sight to the blinde: the Lord rayseth vp the crooked: the Lord loueth the righteous.
9 Yahwe huwalinda wageni katika nchi; huwainua yatima na wajane, bali huipinga njia ya wasio haki.
The Lord keepeth the strangers: he relieueth the fatherlesse and widowe: but he ouerthroweth the way of the wicked.
10 Yahwe atatawala milele, Mungu wako, Sayuni, kwa vizazi vyote. Msifuni Yahwe.
The Lord shall reigne for euer: O Zion, thy God endureth from generation to generation. Prayse ye the Lord.