< Zaburi 145 >

1 Nitakutukuza wewe, Mungu wangu, Mfalme; nitalihimidi jina lako milele na milele.
ダビデのさんびの歌 わが神、王よ、わたしはあなたをあがめ、世々かぎりなくみ名をほめまつります。
2 Kila siku nitakuhimidi; nitalisifu jina lako milele na milele.
わたしは日ごとにあなたをほめ、世々かぎりなくみ名をほめたたえます。
3 Yahwe ndiye mkuu na wakusifiwa sana; ukuu wake hauchunguziki.
主は大いなる神で、大いにほめたたえらるべきです。その大いなることは測り知ることができません。
4 Kizazi kimoja kitayasifu matendo yako kwa kizazi kijacho na kitatangaza matendo yako makuu.
この代はかの代にむかってあなたのみわざをほめたたえ、あなたの大能のはたらきを宣べ伝えるでしょう。
5 Nitaitafakari fahari ya utukufu wa adhama yako na matendo yako ajabu.
わたしはあなたの威厳の光栄ある輝きと、あなたのくすしきみわざとを深く思います。
6 Watanena juu ya nguvu ya kazi zako za kutisha, nami nitatangaza ukuu wako.
人々はあなたの恐るべきはたらきの勢いを語り、わたしはあなたの大いなることを宣べ伝えます。
7 Nao watatangaza wingi wa wema wako, na wataimba kuhusu haki yako.
彼らはあなたの豊かな恵みの思い出を言いあらわし、あなたの義を喜び歌うでしょう。
8 Yahwe ni wa neema na huruma, si mwepesi wa hasira na mwingi katika uaminifu wa agano lake.
主は恵みふかく、あわれみに満ち、怒ることおそく、いつくしみ豊かです。
9 Yahwe ni mwema kwa wote; huruma zake zi juu ya kazi zake zote.
主はすべてのものに恵みがあり、そのあわれみはすべてのみわざの上にあります。
10 Vyote ulivyo viumba vitakushukuru wewe, Yahwe; waaminifu wako watakutukuza wewe.
主よ、あなたのすべてのみわざはあなたに感謝し、あなたの聖徒はあなたをほめまつるでしょう。
11 Waaminifu wako watanena juu ya utukufu wa ufalme wako, na watahubiri juu ya nguvu zako.
彼らはみ国の栄光を語り、あなたのみ力を宣べ、
12 Watayafanya matendo makuu ya Mungu ya julikane na wanadamu na utukufu wa fahari ya ufalme wake.
あなたの大能のはたらきと、み国の光栄ある輝きとを人の子に知らせるでしょう。
13 Ufalme wako ni wa milele, na mamlaka yako ya dumu kizazi hata kizazi.
あなたの国はとこしえの国です。あなたのまつりごとはよろずよに絶えることはありません。
14 Yahwe huwategemeza wote waangukao na huwainua wote walioinama chini.
主はすべて倒れんとする者をささえ、すべてかがむ者を立たせられます。
15 Macho ya wote yanakungoja wewe; nawe huwapa chakula chao kwa wakati sahihi.
よろずのものの目はあなたを待ち望んでいます。あなたは時にしたがって彼らに食物を与えられます。
16 Huufungua mkono wako na hukidhi haja ya kila kiumbe hai.
あなたはみ手を開いて、すべての生けるものの願いを飽かせられます。
17 Yahwe ni mwenye haki katika njia zake zote na neema katika yote afanyayo.
主はそのすべての道に正しく、そのすべてのみわざに恵みふかく、
18 Yahwe yu karibu na wote wamwitao, wale wamwitao yeye katika uaminifu.
すべて主を呼ぶ者、誠をもって主を呼ぶ者に主は近いのです。
19 Hutimiza haja za wale wanao mheshimu yeye; husikia kilio chao na kuwaokoa.
主はおのれを恐れる者の願いを満たし、またその叫びを聞いてこれを救われます。
20 Yahwe huwalinda wale wampendao, lakini atawaangamiza waovu wote.
主はおのれを愛する者をすべて守られるが、悪しき者をことごとく滅ぼされます。
21 Kinywa changu kitazinena sifa za Yahwe; wanadamu wote na walitukuze jina lake takatifu milele na milele.
わが口は主の誉を語り、すべての肉なる者は世々かぎりなくその聖なるみ名をほめまつるでしょう。

< Zaburi 145 >