< Zaburi 142 >

1 Kwa sauti yangu namlilia Yahwe anisaidie; kwa sauti yangu naomba kwa ajili ya neema ya Yahwe.
A maskil of David, while he was in the cave, a prayer. Loudly I cry to the Lord: to the Lord plead loudly for mercy,
2 Namwaga malalamiko yangu mbele zake; ninamwambia shida zangu.
I pour my complaint before him, I tell my troubles to him.
3 Roho yangu inapokuwa dhaifu ndani yangu, wewe unajua mapito yangu. Kwenye njia niipitayo wamenifichia mtego.
When my spirit is faint within me, my path is known to you. In the way I am wont to walk in, they have hidden a trap for me.
4 Natazama kulia kwangu na sioni yeyote anayenijali. Sina pa kukimbilia; hakuna anayejali kuhusu uhai wangu.
I look to the right and the left; but not a friend have I. No place of refuge is left me, not a man to care for me.
5 Nilikuita wewe, Yahwe; nikasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.
So I cry to you, O Lord: I say, “My refuge are you, all I have in the land of the living.”
6 Sikia kuita kwangu, maana nimeshushwa chini sana; uniokoe dhidi ya watesi wangu, maana wana nguvu kuliko mimi.
Attend to my piercing cry, for very weak am I. Save me from those who pursue me, for they are too strong for me.
7 Uitoe nafsi yangu kifungoni ili niweze kulishukuru jina lako. Wenye haki watakusanyika karibu nami kwa sababu umekuwa mwema kwangu.”
Free me from prison, that I may give thanks to your name, for the righteous are patiently waiting till you show your bounty to me.

< Zaburi 142 >