< Zaburi 142 >

1 Kwa sauti yangu namlilia Yahwe anisaidie; kwa sauti yangu naomba kwa ajili ya neema ya Yahwe.
Maschil of David; A Prayer when he was in the cave. I cried unto the LORD with my voice; with my voice unto the LORD did I make my supplication.
2 Namwaga malalamiko yangu mbele zake; ninamwambia shida zangu.
I poured out my complaint before him; I shewed before him my trouble.
3 Roho yangu inapokuwa dhaifu ndani yangu, wewe unajua mapito yangu. Kwenye njia niipitayo wamenifichia mtego.
When my spirit was overwhelmed within me, then thou knewest my path. In the way wherein I walked have they privily laid a snare for me.
4 Natazama kulia kwangu na sioni yeyote anayenijali. Sina pa kukimbilia; hakuna anayejali kuhusu uhai wangu.
I looked on [my] right hand, and beheld, but [there was] no man that would know me: refuge failed me; no man cared for my soul.
5 Nilikuita wewe, Yahwe; nikasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.
I cried unto thee, O LORD: I said, Thou [art] my refuge [and] my portion in the land of the living.
6 Sikia kuita kwangu, maana nimeshushwa chini sana; uniokoe dhidi ya watesi wangu, maana wana nguvu kuliko mimi.
Attend unto my cry; for I am brought very low: deliver me from my persecutors; for they are stronger than I.
7 Uitoe nafsi yangu kifungoni ili niweze kulishukuru jina lako. Wenye haki watakusanyika karibu nami kwa sababu umekuwa mwema kwangu.”
Bring my soul out of prison, that I may praise thy name: the righteous shall compass me about; for thou shalt deal bountifully with me.

< Zaburi 142 >