< Zaburi 142 >

1 Kwa sauti yangu namlilia Yahwe anisaidie; kwa sauti yangu naomba kwa ajili ya neema ya Yahwe.
A Psalme of David, to give instruction, and a prayer, when he was in the cave. I cryed vnto the Lord with my voyce: with my voyce I prayed vnto the Lord.
2 Namwaga malalamiko yangu mbele zake; ninamwambia shida zangu.
I powred out my meditation before him, and declared mine affliction in his presence.
3 Roho yangu inapokuwa dhaifu ndani yangu, wewe unajua mapito yangu. Kwenye njia niipitayo wamenifichia mtego.
Though my spirit was in perplexitie in me, yet thou knewest my path: in the way wherein I walked, haue they priuily layde a snare for me.
4 Natazama kulia kwangu na sioni yeyote anayenijali. Sina pa kukimbilia; hakuna anayejali kuhusu uhai wangu.
I looked vpon my right hand, and beheld, but there was none that would knowe me: all refuge failed me, and none cared for my soule.
5 Nilikuita wewe, Yahwe; nikasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.
Then cryed I vnto thee, O Lord, and sayde, thou art mine hope, and my portion in the land of the liuing.
6 Sikia kuita kwangu, maana nimeshushwa chini sana; uniokoe dhidi ya watesi wangu, maana wana nguvu kuliko mimi.
Hearken vnto my crye, for I am brought very lowe: deliuer me from my persecuters, for they are too strong for me.
7 Uitoe nafsi yangu kifungoni ili niweze kulishukuru jina lako. Wenye haki watakusanyika karibu nami kwa sababu umekuwa mwema kwangu.”
Bring my soule out of prison, that I may prayse thy Name: then shall the righteous come about me, when thou art beneficiall vnto me.

< Zaburi 142 >