< Zaburi 142 >
1 Kwa sauti yangu namlilia Yahwe anisaidie; kwa sauti yangu naomba kwa ajili ya neema ya Yahwe.
An instruction of David; when he was in the cave: a prayer. I cry unto Jehovah with my voice: with my voice unto Jehovah do I make supplication.
2 Namwaga malalamiko yangu mbele zake; ninamwambia shida zangu.
I pour out my plaint before him; I shew before him my trouble.
3 Roho yangu inapokuwa dhaifu ndani yangu, wewe unajua mapito yangu. Kwenye njia niipitayo wamenifichia mtego.
When my spirit was overwhelmed within me, then thou knewest my path. In the way wherein I walked have they hidden a snare for me.
4 Natazama kulia kwangu na sioni yeyote anayenijali. Sina pa kukimbilia; hakuna anayejali kuhusu uhai wangu.
Look on the right hand and see; there is no man that knoweth me: refuge hath failed me; no man careth for my soul.
5 Nilikuita wewe, Yahwe; nikasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.
I cried unto thee, Jehovah; I said, Thou art my refuge, my portion in the land of the living.
6 Sikia kuita kwangu, maana nimeshushwa chini sana; uniokoe dhidi ya watesi wangu, maana wana nguvu kuliko mimi.
Attend unto my cry, for I am brought very low; deliver me from my persecutors, for they are stronger than I.
7 Uitoe nafsi yangu kifungoni ili niweze kulishukuru jina lako. Wenye haki watakusanyika karibu nami kwa sababu umekuwa mwema kwangu.”
Bring my soul out of prison, that I may celebrate thy name. The righteous shall surround me, because thou dealest bountifully with me.