< Zaburi 142 >
1 Kwa sauti yangu namlilia Yahwe anisaidie; kwa sauti yangu naomba kwa ajili ya neema ya Yahwe.
Maschil. Of David. A prayer when he was in the hole of the rock. The sound of my cry went up to the Lord; with my voice I made my prayer for grace to the Lord.
2 Namwaga malalamiko yangu mbele zake; ninamwambia shida zangu.
I put all my sorrows before him; and made clear to him all my trouble.
3 Roho yangu inapokuwa dhaifu ndani yangu, wewe unajua mapito yangu. Kwenye njia niipitayo wamenifichia mtego.
When my spirit is overcome, your eyes are on my goings; nets have been secretly placed in the way in which I go.
4 Natazama kulia kwangu na sioni yeyote anayenijali. Sina pa kukimbilia; hakuna anayejali kuhusu uhai wangu.
Looking to my right side, I saw no man who was my friend: I had no safe place; no one had any care for my soul.
5 Nilikuita wewe, Yahwe; nikasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.
I have made my cry to you, O Lord; I have said, You are my safe place, and my heritage in the land of the living.
6 Sikia kuita kwangu, maana nimeshushwa chini sana; uniokoe dhidi ya watesi wangu, maana wana nguvu kuliko mimi.
Give ear to my cry, for I am made very low: take me out of the hands of my haters, for they are stronger than I.
7 Uitoe nafsi yangu kifungoni ili niweze kulishukuru jina lako. Wenye haki watakusanyika karibu nami kwa sababu umekuwa mwema kwangu.”
Take my soul out of prison, so that I may give praise to your name: the upright will give praise because of me; for you have given me a full reward.