< Zaburi 142 >

1 Kwa sauti yangu namlilia Yahwe anisaidie; kwa sauti yangu naomba kwa ajili ya neema ya Yahwe.
I cry with my voice to Jehovah. With my voice to Jehovah I make supplication.
2 Namwaga malalamiko yangu mbele zake; ninamwambia shida zangu.
I pour out my complaint before him. I show my trouble before him.
3 Roho yangu inapokuwa dhaifu ndani yangu, wewe unajua mapito yangu. Kwenye njia niipitayo wamenifichia mtego.
When my spirit was overwhelmed within me, thou knew my path. In the way in which I walk they have hidden a snare for me.
4 Natazama kulia kwangu na sioni yeyote anayenijali. Sina pa kukimbilia; hakuna anayejali kuhusu uhai wangu.
Look on my right hand, and see, for there is no man who knows me. Refuge has failed me. No man cares for my soul.
5 Nilikuita wewe, Yahwe; nikasema, “Wewe ni kimbilio langu, fungu langu katika nchi ya walio hai.
I cried to thee, O Jehovah. I said, Thou are my refuge, my portion in the land of the living.
6 Sikia kuita kwangu, maana nimeshushwa chini sana; uniokoe dhidi ya watesi wangu, maana wana nguvu kuliko mimi.
Attend to my cry, for I am brought very low. Deliver me from my persecutors, for they are stronger than I.
7 Uitoe nafsi yangu kifungoni ili niweze kulishukuru jina lako. Wenye haki watakusanyika karibu nami kwa sababu umekuwa mwema kwangu.”
Bring my soul out of prison that I may give thanks to thy name. The righteous shall encompass me around, for thou will deal bountifully with me.

< Zaburi 142 >