< Zaburi 141 >

1 Ee Yahwe, ninakulilia wewe; uje upesi kwangu. Unisikilize nikuitapo.
A Psalm of David. LORD, I have called upon thee; make haste unto me: give ear unto my voice, when I call unto thee.
2 Maombi yangu na yawe kama uvumba mbele zako; mikono yangu iliyoinuliwa na iwe kama dhabihu ya jioni.
Let my prayer be set forth as incense before thee; the lifting up of my hands as the evening sacrifice.
3 Ee Yahwe, uweke mlinzi kinywani mwangu; mngojezi malangoni pa midomo yangu.
Set a watch, O LORD, before my mouth; keep the door of my tips.
4 Usiruhusu tamaa ya moyo wangu kutamani uovu wowote wala kushiriki katika matendo ya dhambi na watu waishio maovuni. Nisile vyakula vyao vya anasa.
Incline not my heart to any evil thing, to be occupied in deeds of wickedness with men that work iniquity: and let me not eat of their dainties.
5 Mwenye haki na anipige; nao utakuwa ni wema kwangu. Anirudi; itakuwa kama mafuta kichwani pangu; kichwa changu na kisikatae kupokea. Lakini maombi yangu siku zote yatakuwa dhidi ya matendo yao mauvu.
Let the righteous smite me, [it shall be] a kindness; and let him reprove me, [it shall be as] oil upon the head; let not my head refuse it: for even in their wickedness shall my prayer continue.
6 Viongozi wao watatupwa chini toka juu mlimani; watayasikia maneno yangu kuwa ni matamu.
Their judges are thrown down by the sides of the rock; and they shall hear my words; for they are sweet.
7 Watalazimika kusema, “Kama vile jembe moja livunjapo ardhi, hivyo mifupa yetu imesambaratishwa kinywani pa kuzimu.” (Sheol h7585)
As when one ploweth and cleaveth the earth, our bones are scattered at the grave’s mouth. (Sheol h7585)
8 Hakika macho yangu yanakutazama wewe, Yahwe, Bwana; katika wewe napata kimbilio; usiiache nafsi yangu.
For mine eyes are unto thee, O GOD the Lord: in thee do I put my trust; leave not my soul destitute.
9 Unilinde dhidi ya mitego waliyoiweka kwa ajili yangu, na matanzi yao watendao maovu.
Keep me from the snare which they have laid for me, and from the gins of the workers of iniquity.
10 Waovu na waangukie kwenye nyavu zao wenywe pindi mimi nitorokapo.
Let the wicked fall into their own nets, whilst that I withal escape.

< Zaburi 141 >