< Zaburi 141 >

1 Ee Yahwe, ninakulilia wewe; uje upesi kwangu. Unisikilize nikuitapo.
LORD, I cry unto thee: make haste unto me; give ear unto my voice, when I cry unto thee.
2 Maombi yangu na yawe kama uvumba mbele zako; mikono yangu iliyoinuliwa na iwe kama dhabihu ya jioni.
Let my prayer be set forth before thee as incense; and the lifting up of my hands as the evening sacrifice.
3 Ee Yahwe, uweke mlinzi kinywani mwangu; mngojezi malangoni pa midomo yangu.
Set a watch, O Lord, before my mouth; keep the door of my lips.
4 Usiruhusu tamaa ya moyo wangu kutamani uovu wowote wala kushiriki katika matendo ya dhambi na watu waishio maovuni. Nisile vyakula vyao vya anasa.
Incline not my heart to any evil thing, to practise wicked works with men that work iniquity: and let me not eat of their dainties.
5 Mwenye haki na anipige; nao utakuwa ni wema kwangu. Anirudi; itakuwa kama mafuta kichwani pangu; kichwa changu na kisikatae kupokea. Lakini maombi yangu siku zote yatakuwa dhidi ya matendo yao mauvu.
Let the righteous smite me; it shall be a kindness: and let him reprove me; it shall be an excellent oil, which shall not break my head: for yet my prayer also shall be in their calamities.
6 Viongozi wao watatupwa chini toka juu mlimani; watayasikia maneno yangu kuwa ni matamu.
When their judges are overthrown in stony places, they shall hear my words; for they are sweet.
7 Watalazimika kusema, “Kama vile jembe moja livunjapo ardhi, hivyo mifupa yetu imesambaratishwa kinywani pa kuzimu.” (Sheol h7585)
Our bones are scattered at the grave’s mouth, as when one cutteth and cleaveth wood upon the earth. (Sheol h7585)
8 Hakika macho yangu yanakutazama wewe, Yahwe, Bwana; katika wewe napata kimbilio; usiiache nafsi yangu.
But mine eyes are unto thee, O God the Lord: in thee is my trust; leave not my soul destitute.
9 Unilinde dhidi ya mitego waliyoiweka kwa ajili yangu, na matanzi yao watendao maovu.
Keep me from the snares which they have laid for me, and the gins of the workers of iniquity.
10 Waovu na waangukie kwenye nyavu zao wenywe pindi mimi nitorokapo.
Let the wicked fall into their own nets, whilst that I withal escape.

< Zaburi 141 >