< Zaburi 138 >
1 Nitakushukuru kwa moyo wangu wote; mbele ya miungu nitakuimbia sifa.
[A Psalm] of David. I will give thee thanks with my whole heart: before the gods will I sing praises unto thee.
2 Nitasujundu mbele ya hekalu lako takatifu na kulishukuru jina lako kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na kwa uaminifu wako. Umelifanya muhimu zaidi neno lako na jina lako kuliko kitu chochote.
I will worship toward thy holy temple, and give thanks unto thy name for thy lovingkindness and for thy truth: for thou hast magnified thy word above all thy name.
3 Siku ile niliyo kuita, ulinijibu; ulinitia moyo na kuitia nguvu nafsi yangu.
In the day that I called thou answeredst me, thou didst encourage me with strength in my soul.
4 Wafalme wote wa nchi watakushukuru wewe, Yahwe, maana watasikia maneno kutoka kinywani mwako.
All the kings of the earth shall give thee thanks, O LORD, for they have heard the words of thy mouth.
5 Hakika, wataimba kuhusu matendo ya Yahwe, kwa kuwa utukufu wa Yahwe ni mkuu.
Yea, they shall sing of the ways of the LORD; for great is the glory of the LORD.
6 Maana ingawa Yahwe yuko juu, lakini anawajali wanyenyekevu, lakini hawatambui wenye majivuno.
For though the LORD be high, yet hath he respect unto the lowly: but the haughty he knoweth from afar.
7 Nijapopita katikati ya hatari, wewe utauhifadhi uhai wangu; utanyoosha mkono wako dhidi ya hasira ya adui zangu, na mkono wako wa kuume utaniokoa.
Though I walk in the midst of trouble, thou wilt revive me; thou shalt stretch forth thine hand against the wrath of mine enemies, and thy right hand shall save me.
8 Yahwe yuko pamoja nami hadi mwisho; uaminifu wa agano lako, Yahwe, wadumu milele. Usiwaache wale ambao mikono yako imewaumba.
The LORD will perfect that which concerneth me: thy mercy, O LORD, [endureth] for ever; forsake not the works of thine own hands.