< Zaburi 137 >
1 Kando ya mito ya Babeli tuliketi na tulilia tulipokumbuka kuhusu Sayuni.
An den Strömen Babels, da saßen wir und weinten, indem wir Zions gedachten.
2 Tulitundika vinubi vyetu kwenye miti ya Babylon.
An den Weiden, die dort waren, hingen wir unsere Zithern auf.
3 Huko watekaji wetu walitaka tuwaimbie, na wale walio tudhihaki walitutaka sisi tufurahi, wakisema, “Tuimbieni moja ya nyimbo za Sayuni.”
Denn dort begehrten, die uns gefangen geführt, Lieder von uns, und unsere Peiniger Fröhlichkeit: “Singt uns eines von den Zionsliedern!”
4 Tungewezaje kuimba wimbo unaomuhusu Yahwe katika nchi ya ugeni?
Wie könnten wir die Jahwe-Lieder singen auf dem Boden der Fremde!
5 Kama nikikusahau wewe, Yerusalemu, basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
Wenn ich deiner vergesse, Jerusalem, so schrumpfe meine Rechte ein.
6 Ulimi wangu na ushikamane juu ya kinywa changu kama nisipokufikiria tena, na kama sipendelei zaidi Yerusalemu kuliko furaha yangu kuu.
Es klebe meine Zunge an meinem Gaumen, wenn ich deiner nicht gedenke, wenn ich nicht lasse Jerusalem meine höchste Freude sein!
7 Kumbuka, Ee Yahwe, kile walichofanya Waedomu siku ya anguko la Yerusalemu. Walisema, “Ibomoeni, ibomoeni mpaka chini kwenye misingi yake.”
Gedenke, Jahwe, den Edomitern, den Unglückstag Jerusalems, die da riefen: “Nieder damit, nieder damit bis auf den Grund in ihr!”
8 Binti za Babeli, hivi karibuni wataharibiwa- mtu na abalikiwe, yeyote atakaye walipizia yale mliotufanyia sisi.
Tochter Babel, du Verwüsterin, wohl dem, der dir vergilt, was du uns angethan!
9 Mtu na abarikiwe, yeyote achukuaye na kusambaratisha watoto wenu juu ya jiwe.
Wohl dem, der deine zarten Kinder packt und schmettert an den Felsen.