< Zaburi 137 >

1 Kando ya mito ya Babeli tuliketi na tulilia tulipokumbuka kuhusu Sayuni.
An den Flüssen Babels, daß saßen wir und weinten, / Wenn wir an Zion gedachten.
2 Tulitundika vinubi vyetu kwenye miti ya Babylon.
An den Weiden, die dort standen, / Hingen wir unsre Zithern auf.
3 Huko watekaji wetu walitaka tuwaimbie, na wale walio tudhihaki walitutaka sisi tufurahi, wakisema, “Tuimbieni moja ya nyimbo za Sayuni.”
Denn da wollten unsre Sieger von uns Lieder hören / Und unsre Quäler Freudengesang. / "Singt uns", so riefen sie (höhnisch), / "eins von den Zionsliedern!"
4 Tungewezaje kuimba wimbo unaomuhusu Yahwe katika nchi ya ugeni?
Wie sollten wir Jahwes Lieder singen / In einem fremden Lande?
5 Kama nikikusahau wewe, Yerusalemu, basi mkono wangu wa kuume na usahau ujuzi wake.
Vergeß ich dein Jerusalem, / So sterbe mir ab meine rechte Hand!
6 Ulimi wangu na ushikamane juu ya kinywa changu kama nisipokufikiria tena, na kama sipendelei zaidi Yerusalemu kuliko furaha yangu kuu.
Meine Zunge klebe an meinem Gaumen, / Wenn ich nicht dein gedenke, / Wenn mir nicht Jerusalem / Meine höchste Freude ist.
7 Kumbuka, Ee Yahwe, kile walichofanya Waedomu siku ya anguko la Yerusalemu. Walisema, “Ibomoeni, ibomoeni mpaka chini kwenye misingi yake.”
Gedenke, o Jahwe, Edoms Söhnen / Den Tag Jerusalems, / Die da riefen: "Nieder, nieder mit ihr / Bis auf den Grund!"
8 Binti za Babeli, hivi karibuni wataharibiwa- mtu na abalikiwe, yeyote atakaye walipizia yale mliotufanyia sisi.
O Tochter Babels, du Zwingherrin, wohl dem, der dir vergelten wird / All das, was du an uns verübt!
9 Mtu na abarikiwe, yeyote achukuaye na kusambaratisha watoto wenu juu ya jiwe.
Wohl dem, der deine jungen Kinder ergreift / Und sie am Felsen zerschmettert!

< Zaburi 137 >