< Zaburi 136 >

1 Oh, mshukuruni Yahwe; kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Alleluya. Knouleche ye to the Lord, for he is good, for his merci is withouten ende.
2 Oh, Mshukuruni Mungu wa miungu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Knouleche ye to the God of goddis.
3 Oh, mshukuruni Bwana wa mabwana, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Knouleche ye to the Lord of lordis.
4 Mshukuruni yeye ambaye peke yake hufanya maajabu makuu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Which aloone makith grete merueils.
5 Yeye aliyezifanya mbingu kwa hekima zake, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Which made heuenes bi vndurstondyng.
6 Mshukuruni yeye alitetandaza nchi juu ya maji, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Which made stidefast erthe on watris.
7 Yeye aliyefanya mianga mikubwa, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Which made grete liytis.
8 Mshukuruni yeye alipaye jua kutawala mchana, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
The sunne in to the power of the dai.
9 Mwezi na nyota vitawale usiku, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
The moone and sterris in to the power of the niyt.
10 Mshukuruni yeye aliyewaua wazaliwa wa kwanza wa Misri, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Which smoot Egipt with the firste gendrid thingis of hem.
11 Akawatoa Waisraeli kati yao, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Which ledde out Israel fro the myddil of hem.
12 Kwa mkono hodari na mkono ulio nyooshwa, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
In a miyti hond and in an hiy arm.
13 Mshukuruni yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Whiche departide the reed see in to departyngis.
14 Na kuwapitisha Waisraeli katikati yake, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
And ledde out Israel thoruy the myddil therof.
15 Lakini akamtupa Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
And he `caste a down Farao and his pouer in the reed see.
16 Mshukuruni yeye aliye waongoza watu wake jangwani, kwa maana uaminifu wa agano lake ni wa milele.
Which ledde ouer his puple thoruy desert.
17 Yeye aliyewaua wafalme wakuu, kwa maana uaminifu wa agano lake ni wadumu milele.
Which smoot grete kingis.
18 Mshukuruni yeye aliyewaua wafalme maarufu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
And killide strong kingis.
19 Sihoni mfalme wa Waamori, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Seon, the king of Amorreis.
20 Na Ogu, mfalme wa Bashani, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
And Og, the king of Baasan.
21 Mshukuruni yeye aliyewapa nchi yao kama urithi, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
And he yaf the lond of hem eritage.
22 Urithi wa Israel mtumishi wake, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Eritage to Israel, his seruaunt.
23 Yeye aliyetukumbuka na kutusaidia katika unyonge wetu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
For in oure lownesse he hadde mynde on vs.
24 Mshukuruni yeye ambaye ametupa ushindi juu ya aui zetu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
And he ayenbouyte vs fro oure enemyes.
25 Yeye awapaye chakula viumbe hai wote, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Which yyueth mete to ech fleisch. Knouleche ye to God of heuene.
26 Oh, mshukuruni Mungu wa mbinguni, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Knouleche ye to the Lord of lordis; for his merci is with outen ende.

< Zaburi 136 >