< Zaburi 136 >

1 Oh, mshukuruni Yahwe; kwa kuwa ni mwema, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Give thanks to the LORD, for He is good.
2 Oh, Mshukuruni Mungu wa miungu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Give thanks to the God of gods.
3 Oh, mshukuruni Bwana wa mabwana, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Give thanks to the Lord of lords.
4 Mshukuruni yeye ambaye peke yake hufanya maajabu makuu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
He alone does great wonders.
5 Yeye aliyezifanya mbingu kwa hekima zake, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
By His insight He made the heavens.
6 Mshukuruni yeye alitetandaza nchi juu ya maji, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
He spread out the earth upon the waters.
7 Yeye aliyefanya mianga mikubwa, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
He made the great lights—
8 Mshukuruni yeye alipaye jua kutawala mchana, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
the sun to rule the day,
9 Mwezi na nyota vitawale usiku, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
the moon and stars to govern the night.
10 Mshukuruni yeye aliyewaua wazaliwa wa kwanza wa Misri, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
He struck down the firstborn of Egypt
11 Akawatoa Waisraeli kati yao, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
and brought Israel out from among them
12 Kwa mkono hodari na mkono ulio nyooshwa, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
with a mighty hand and an outstretched arm.
13 Mshukuruni yeye aliyeigawa Bahari ya Shamu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
He divided the Red Sea in two
14 Na kuwapitisha Waisraeli katikati yake, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
and led Israel through the midst,
15 Lakini akamtupa Farao na jeshi lake katika Bahari ya Shamu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
but swept Pharaoh and his army into the Red Sea.
16 Mshukuruni yeye aliye waongoza watu wake jangwani, kwa maana uaminifu wa agano lake ni wa milele.
He led His people through the wilderness.
17 Yeye aliyewaua wafalme wakuu, kwa maana uaminifu wa agano lake ni wadumu milele.
He struck down great kings
18 Mshukuruni yeye aliyewaua wafalme maarufu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
and slaughtered mighty kings—
19 Sihoni mfalme wa Waamori, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Sihon king of the Amorites
20 Na Ogu, mfalme wa Bashani, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
and Og king of Bashan—
21 Mshukuruni yeye aliyewapa nchi yao kama urithi, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
and He gave their land as an inheritance,
22 Urithi wa Israel mtumishi wake, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
a heritage to His servant Israel.
23 Yeye aliyetukumbuka na kutusaidia katika unyonge wetu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
He remembered us in our low estate
24 Mshukuruni yeye ambaye ametupa ushindi juu ya aui zetu, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
and freed us from our enemies.
25 Yeye awapaye chakula viumbe hai wote, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
He gives food to every creature.
26 Oh, mshukuruni Mungu wa mbinguni, kwa maana uaminifu wa agano lake wadumu milele.
Give thanks to the God of heaven!

< Zaburi 136 >