< Zaburi 135 >

1 Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
Louvae ao Senhor. Louvae o nome do Senhor; louvae-o, servos do Senhor.
2 ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Vós que assistis na casa do Senhor, nos atrios da casa do nosso Deus.
3 Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
Louvae ao Senhor, porque o Senhor é bom: cantae louvores ao seu nome, porque é agradavel.
4 Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
Porque o Senhor escolheu para si a Jacob, e a Israel para seu proprio thesouro.
5 Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
Porque eu conheço que o Senhor é grande e que o nosso Deus está acima de todos os deuses.
6 Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
Tudo o que o Senhor quiz fez, nos céus e na terra, nos mares e em todos os abysmos.
7 Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
Faz subir os vapores das extremidades da terra; faz os relampagos para a chuva; produz os ventos dos seus thesouros.
8 Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
O que feriu os primogenitos do Egypto, desde os homens até ás bestas.
9 Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
O que enviou signaes e prodigios no meio de ti, ó Egypto, contra Pharaó e contra os seus servos.
10 Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
O que feriu muitas nações, e matou poderosos reis;
11 Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
A Sehon, rei dos amorrheos, e a Og, rei de Basan, e a todos os reinos de Canaan.
12 Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
E deu a sua terra em herança, em herança a Israel, seu povo.
13 Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
O teu nome, ó Senhor, dura perpetuamente; e a tua memoria, ó Senhor, de geração em geração.
14 Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
Pois o Senhor julgará o seu povo, e se arrependerá com respeito aos seus servos.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Os idolos das nações são prata e oiro, obra das mãos dos homens.
16 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
Teem bocca, mas não fallam; teem olhos, e não vêem.
17 zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
Teem ouvidos, mas não ouvem, nem ha respiro algum nas suas boccas.
18 Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
Similhantes a elles se tornem os que os fazem, e todos os que confiam n'elles.
19 Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
Casa d'Israel, bemdizei ao Senhor; casa d'Aarão bemdizei ao Senhor.
20 Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
Casa de Levi, bemdizei ao Senhor: vós, os que temeis ao Senhor, louvae ao Senhor.
21 Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
Bemdito seja o Senhor desde Sião, que habita em Jerusalem. Louvae ao Senhor.

< Zaburi 135 >