< Zaburi 135 >

1 Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
Halleluja. Chwalcie imię Pańskie, chwalcie słudzy Pańscy.
2 ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Którzy stawacie w domu Pańskim, w sieniach domu Boga naszego.
3 Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
Chwalcież Pana, albowiem to Pan dobry; śpiewajcież imieniowi jego, boć jest wdzięczne.
4 Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
Albowiem sobie Jakóba Pan obrał, i Izraela za własność swoję.
5 Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
Jać zaiste uznaję, iż wielki jest Pan, a Pan nasz jest nad wszystkich bogów.
6 Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
Wszystko co chce Pan, to czyni, na niebie i na ziemi, w morzu i we wszystkich przepaściach.
7 Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
Który czyni, że występują pary od kończyn ziemi; błyskawice i dżdże przywodzi, wywodzi wiatr z skarbów swoich;
8 Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
Który pobił pierworodztwa w Egipcie, od człowieka aż do bydlęcia.
9 Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Posłał znaki i cuda w pośród ciebie, Egipcie! na Faraona i na wszystkich sług jego.
10 Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
Który poraził wiele narodów, a pobił królów możnych;
11 Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
Sehona, króla Amorejskiego, i Oga, króla Basańskiego, i wszystkie królestwa Chananejskie.
12 Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
I dał ziemię ich w dziedzictwo, w dziedzictwo Izraelowi, ludowi swemu.
13 Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
Panie! imię twoje na wieki; Panie! pamiątka twoja od narodu do narodu.
14 Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
Zaite Pan sądzić będzie lud swój, a nad sługami swymi zmiłuje się.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Ale bałwany pogańskie, srebro i złoto, są robotą rąk ludzkich.
16 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
Usta mają, a nie mówią, oczy mają, a nie widzą;
17 zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
Uszy mają, a nie słyszą, ani mają tchnienia w ustach swoich.
18 Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
Niech im podobni będą, którzy je robią, i wszyscy, którzy w nich ufają.
19 Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
Domie Izraelski! błogosławcie Panu; domie Aaronowy! błogosławcie Panu.
20 Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
Domie Lewiego! błogosławcie Panu, którzy się boicie Pana, błogosławcie Panu.
21 Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
Błogosławiony Pan z Syonu, który mieszka w Jeruzalemie. Halleluja.

< Zaburi 135 >