< Zaburi 135 >
1 Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
ALLELUIA. Lodate il Nome del Signore; Lodate[lo, voi] servitori del Signore;
2 ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Che state nella Casa del Signore, Ne' cortili della Casa del nostro Dio.
3 Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
Lodate il Signore; perciocchè il Signore [è] buono; Salmeggiate al suo Nome, perciocchè [è] amabile.
4 Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
Conciossiachè il Signore si abbia eletto Giacobbe [Ed] Israele per suo tesoro riposto.
5 Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
Certo io conosco che il Signore [è] grande, E che il nostro Signore [è maggiore] di tutti gl'iddii.
6 Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
Il Signore fa tutto ciò che gli piace In cielo ed in terra; Ne' mari, ed [in] tutti gli abissi.
7 Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
Egli fa salire i vapori dall'estremità dalle terra; Egli fa i lampi per la pioggia; Egli trae fuori il vento da' suoi tesori.
8 Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
[Egli è quel] che percosse i primogeniti di Egitto, Così degli uomini, come degli animali.
9 Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Che mandò segni e prodigi, in mezzo di te, o Egitto; Sopra Faraone, e sopra tutti i suoi servitori.
10 Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
Che percosse nazioni grandi, Ed uccise re potenti;
11 Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
Sihon, re degli Amorrei, E Og, re di Basan, E i re di tutti i regni di Canaan;
12 Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
E diede i lor paesi per eredità, Per eredità ad Israele, suo popolo.
13 Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
O Signore, il tuo Nome [è] in eterno; O Signore, la memoria di te [è] per ogni età.
14 Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
Quando il Signore avrà fatti i suoi giudicii sopra il suo popolo, Egli si pentirà per amor de' suoi servitori.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Gl'idoli delle genti[sono] argento ed oro, Opera di mani d'uomini;
16 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
Hanno bocca, e non parlano; Hanno occhi, e non veggono;
17 zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
Hanno orecchi, e non odono; [Ed] anche non hanno fiato alcuno nella lor bocca.
18 Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
Simili ad essi sieno quelli che li fanno; Chiunque in essi si confida.
19 Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
Casa d'Israele, benedite il Signore; Casa d'Aaronne, benedite il Signore.
20 Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
Casa di Levi, benedite il Signore; [Voi] che temete il Signore, beneditelo.
21 Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
Benedetto [sia] da Sion il Signore, Che abita in Gerusalemme. Alleluia.