< Zaburi 135 >

1 Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
הללו יה הללו את שם יהוה הללו עבדי יהוה׃
2 ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
שעמדים בבית יהוה בחצרות בית אלהינו׃
3 Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
הללו יה כי טוב יהוה זמרו לשמו כי נעים׃
4 Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
כי יעקב בחר לו יה ישראל לסגלתו׃
5 Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
כי אני ידעתי כי גדול יהוה ואדנינו מכל אלהים׃
6 Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
כל אשר חפץ יהוה עשה בשמים ובארץ בימים וכל תהומות׃
7 Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
מעלה נשאים מקצה הארץ ברקים למטר עשה מוצא רוח מאוצרותיו׃
8 Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
שהכה בכורי מצרים מאדם עד בהמה׃
9 Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
שלח אתות ומפתים בתוככי מצרים בפרעה ובכל עבדיו׃
10 Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
שהכה גוים רבים והרג מלכים עצומים׃
11 Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
לסיחון מלך האמרי ולעוג מלך הבשן ולכל ממלכות כנען׃
12 Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
ונתן ארצם נחלה נחלה לישראל עמו׃
13 Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
יהוה שמך לעולם יהוה זכרך לדר ודר׃
14 Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
כי ידין יהוה עמו ועל עבדיו יתנחם׃
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
עצבי הגוים כסף וזהב מעשה ידי אדם׃
16 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
פה להם ולא ידברו עינים להם ולא יראו׃
17 zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
אזנים להם ולא יאזינו אף אין יש רוח בפיהם׃
18 Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
כמוהם יהיו עשיהם כל אשר בטח בהם׃
19 Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
בית ישראל ברכו את יהוה בית אהרן ברכו את יהוה׃
20 Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
בית הלוי ברכו את יהוה יראי יהוה ברכו את יהוה׃
21 Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
ברוך יהוה מציון שכן ירושלם הללו יה׃

< Zaburi 135 >