< Zaburi 135 >

1 Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
Lobet Jehova! Lobet den Namen Jehovas! Lobet, ihr Knechte Jehovas,
2 ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
die ihr stehet im Hause Jehovas, in den Vorhöfen des Hauses unseres Gottes!
3 Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
Lobet Jehova! Denn gut ist Jehova; singet Psalmen seinem Namen! Denn er ist lieblich.
4 Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
Denn Jehova hat sich Jakob erwählt, Israel zu seinem Eigentum.
5 Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
Denn ich weiß, daß Jehova groß ist, und unser Herr groß vor allen Göttern.
6 Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
Alles, was Jehova wohlgefällt, tut er in den Himmeln und auf der Erde, in den Meeren und in allen Tiefen;
7 Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
der Dünste aufsteigen läßt vom Ende der Erde, der Blitze macht zum Regen, der den Wind herausführt aus seinen Vorratskammern;
8 Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
der die Erstgeborenen Ägyptens schlug vom Menschen bis zum Vieh,
9 Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Zeichen und Wunder sandte in deine Mitte, Ägypten, wider den Pharao und wider alle seine Knechte;
10 Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
der große Nationen schlug und starke Könige tötete:
11 Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
Sihon, den König der Amoriter, und Og, den König von Basan, und alle Königreiche Kanaans;
12 Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
und ihr Land als Erbteil gab, als Erbteil seinem Volke Israel.
13 Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
Jehova, dein Name währt ewiglich, Jehova, dein Gedächtnis von Geschlecht zu Geschlecht.
14 Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
Denn Jehova wird sein Volk richten, und er wird sich's gereuen lassen über seine Knechte.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Die Götzen der Nationen sind Silber und Gold, ein Werk von Menschenhänden.
16 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
Einen Mund haben sie und reden nicht; Augen haben sie und sehen nicht;
17 zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
Ohren haben sie und hören nicht; auch ist kein Odem in ihrem Munde.
18 Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
Ihnen gleich sind die, die sie machen, ein jeder, der auf sie vertraut.
19 Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
Haus Israel, preiset Jehova! Haus Aaron, preiset Jehova!
20 Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
Haus Levi, preiset Jehova! Die ihr Jehova fürchtet, preiset Jehova!
21 Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
Gepriesen sei Jehova von Zion aus, der zu Jerusalem wohnt! Lobet Jehova!

< Zaburi 135 >