< Zaburi 135 >

1 Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
Lobet Jah! / Lobt den Namen Jahwes, / Lobt ihn, ihr Knechte Jahwes,
2 ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
Die ihr steht in Jahwes Haus, / In den Höfen des Hauses unsers Gottes!
3 Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
Lobt Jah, denn Jahwe ist gütig, / Spielt seinem Namen, denn lieblich ist er!
4 Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
Denn Jah hat Jakob erkoren, / Israel sich zum Eigentum erwählt.
5 Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
Denn ich weiß wohl, daß Jahwe groß ist / Und unser Herr alle Götter überragt.
6 Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
Alles, was Jahwe gefiel, das hat er gemacht / Im Himmel und auf Erden, / In den Meeren und allen Tiefen.
7 Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
Er führt Wolken herauf vom Ende der Erde, / Läßt künden durch Blitze Gewitterregen, / Holt Wind aus seinen Speichern hervor.
8 Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
Er schlug Ägyptens Erstgeburten / Von Menschen bis zum Vieh.
9 Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Er sandte Zeichen und Wunder / Wider dich, Ägyptenland, / Wider Pharao und all seine Knechte.
10 Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
Er schlug viele Völker / Und tötete mächtige Könige.
11 Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
Sihon, der Amoriter König, / Und Og, den König von Basan, / Ja, machte zunichte alle Reiche Kanaans.
12 Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
Er gab ihr Land als Erbe, / Als Erbe Israel, seinem Volk.
13 Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
Jahwe, dein Name währt ewig; / Dein Gedächtnis, Jahwe, bleibt für und für.
14 Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
Denn Jahwe wird seinem Volk Recht schaffen / Und mit seinen Knechten Erbarmen haben.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Der Heiden Götzen sind Silber und Gold, / Das Gebilde von Menschenhand.
16 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
Sie haben einen Mund und können nicht reden, / Sie haben Augen und sehen doch nicht.
17 zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
Ohren haben sie und hören nicht, / Noch haben sie Odem in ihrem Mund.
18 Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
Ihnen gleich sind, die sie bilden — / Jeder, der ihnen vertraut.
19 Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
Ihr von Israels Haus, preist Jahwe! / Ihr von Aarons Haus, preist Jahwe!
20 Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
Ihr von Levis Haus, preist Jahwe! / Die ihr Jahwe fürchtet, preist Jahwe!
21 Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
Gepriesen sei Jahwe von Zion aus, / Er, der in Jerusalem wohnt. / Lobt Jah!

< Zaburi 135 >