< Zaburi 135 >

1 Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
Alleluia. Louez le nom de Yahweh, louez-le, serviteurs de Yahweh,
2 ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
vous qui êtes de service dans la maison de Yahweh, dans les parvis de la maison de notre Dieu.
3 Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
Louez Yahweh, car Yahweh est bon; chantez son nom sur la harpe, car il est plein de douceur.
4 Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
Car Yahweh s’est choisi Jacob, il s’est choisi Israël pour en faire son héritage.
5 Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
Oui, je le sais, Yahweh est grand, notre Seigneur est au-dessus de tous les dieux.
6 Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
Tout ce que veut Yahweh, il le fait, dans les cieux et sur la terre, dans la mer et dans tous les abîmes.
7 Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
Il fait monter les nuages des extrémités de la terre, il produit les éclairs avec la pluie, il tire le vent de ses trésors.
8 Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
Il frappa jadis les premiers-nés de l’Égypte, depuis l’homme jusqu’à l’animal.
9 Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
Il fit éclater des signes et des prodiges au milieu de toi, ô Égypte, contre Pharaon et tous ses serviteurs.
10 Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
Il frappa des nations nombreuses, et fit mourir des rois puissants:
11 Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
Séhon, roi des Amorrhéens, Og, roi de Basan, et tous les rois de Canaan.
12 Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
Et il donna leur pays en héritage, en héritage à Israël, son peuple.
13 Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
Yahweh, ton nom subsiste à jamais; Yahweh, ton souvenir dure d’âge en âge.
14 Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
Car Yahweh fait droit à son peuple, et il a compassion de ses serviteurs.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Les idoles des nations sont de l’argent et de l’or, ouvrage de la main des hommes.
16 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
Elles ont une bouche et ne parlent pas; elles ont des yeux et ne voient pas.
17 zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
Elles ont des oreilles et n’entendent pas; Il n’y a pas même un souffle dans leur bouche.
18 Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
Qu’ils leur ressemblent ceux qui les font, quiconque se confie en elles!
19 Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
Maison d’Israël, bénissez Yahweh! Maison d’Aaron, bénissez Yahweh!
20 Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
Maison de Lévi, bénissez Yahweh! Vous qui craignez Yahweh, bénissez Yahweh!
21 Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
Que de Sion soit béni Yahweh, qui habite Jérusalem! Alleluia!

< Zaburi 135 >