< Zaburi 135 >

1 Msifuni Yahwe. Lisifuni jina la Yahwe. Msifuni yeye, enyi watumishi wa Yahwe,
Lover Herrens Navn, lover, I Herrens Tjenere!
2 ninyi msimamao katika nyumba ya Yahwe, katika nyua za nyumba ya Mungu wetu.
I, som staa i Herrens Hus, i vor Guds Hus's Forgaarde.
3 Msifuni Yahwe, kwa kuwa ni mwema; liimbieni sifa jina lake, maana ni vizuri kufanya hivyo.
Lover Herren; thi Herren er god; lovsynger hans Navn; thi det er lifligt.
4 Kwa kuwa Yahwe amemchagua Yakobo kwa ajili yake mwenyewe, Israeli kama urithi wake.
Thi Herren har udvalgt sig Jakob, Israel til sin Ejendom.
5 Najua ya kuwa Yahwe ni mkuu, na kwamba Bwana wetu yuko juu ya miungu yote.
Thi jeg ved, at Herren er stor, og at vor Herre er større end alle Guder.
6 Chochote Yahwe apendacho, hufanya mbinguni, duniani, katika bahari na katika vilindi vyote.
Herren gør alt, hvad ham behager, i Himmelen og paa Jorden, i Havene og i alle Afgrunde.
7 Hushusha mawingu kutoka mbali, akifanya mianga ya radi kuongozana na mvua na kuleta upepo toka katika ghala yake.
Han gør, at Dampe opstige fra Jordens Grænse; han gør Lynene til Regn, han udfører Vejret af sine Forraadskamre.
8 Aliua mzaliwa wa kwanza wa Misri, wote wanadamu na wanyama.
Han, som slog de førstefødte i Ægypten, baade Mennesker og Dyr;
9 Alituma ishara na maajabu kati yako Misri, dhidi ya Farao na watumishi wake wote.
han sendte Tegn og underlige Ting i din Midte, Ægypten! paa Farao og paa alle hans Tjenere;
10 Aliwashambulia mataifa mengi na aliua wafalme wenye nguvu,
han, som slog mange Folk og ihjelslog stærke Konger:
11 Sihoni mfalme wa Waamori na Ogu mfalme wa Bashani na falme zote za Kanaani.
Amoriternes Konge Sihon og Basans Konge Og samt alle Riger i Kanaan;
12 Alitupatia sisi nchi yao kama urithi, urithi wa Israeli watu wake.
og han gav deres Land til Arv, til Arv for sit Folk Israel.
13 Jina lako, Yahwe, inadumu milele; Yahwe, kumbukumbu lako vizazi hata vizazi.
Herre! dit Navn bliver evindelig; Herre! din Ihukommelse bliver fra Slægt til Slægt.
14 Kwa kuwa Bwana huwatetea watu wake na anahuruma juu ya watumishi wake.
Thi Herren skal dømme sit Folk, og det skal angre ham for hans Tjeneres Skyld.
15 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Hedningernes Afguder ere Sølv og Guld, et Menneskes Hænders Gerning.
16 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
De have Mund, men tale ikke; de have Øjne, men se ikke.
17 zina masikio, lakini hazisikii, wala vinywani mwao hamna pumzi.
De have Øren, men høre ikke, og der er ingen Aande i deres Mund.
18 Wale wazitengenezao wanafanana nazo, vilevile kila anaye zitumainia.
Ligesom disse ere, saa blive de, som gøre dem, ja, hver den, som forlader sig paa dem.
19 Enyi kizazi cha Israeli, mtukuzeni Yahwe; kizazi cha Haruni, mtukuzeni Yahwe.
Israels Hus! lover Herren; Arons Hus! lover Herren.
20 Kizazi cha Lawi, mtukuzeni Yahwe.
Levis Hus! lover Herren; I, som frygte Herren! lover Herren.
21 Atukuzwe Yahwe katika Sayuni, yeye aishiye Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
Lovet være Herren fra Zion, han, som bor i Jerusalem! Halleluja!

< Zaburi 135 >