< Zaburi 13 >
1 Mpaka lini, Yahweh, utaendelea kunisahau? Ni kwa muda gani utauficha uso wako nisiuone?
(Til sangmesteren. En salme af David.) Hvor længe vil du evigt glemme mig, Herre, hvor længe skjule dit Åsyn for mig?
2 Ni kwa muda gani nitalazimika kuhofu na kuhuzunika moyoni mwangu kila siku? Ni kwa muda gani adui zangu watanishida?
Hvor længe skal jeg huse Sorg i min Sjæl, Kvide i Hjertet Dag og Nat? Hvor længe skal Fjenden ophøje sig over mig?
3 Unitazame na unijibu, Yahwe Mungu wangu! Nipe mwanga machoni pangu, vinginevyo nitalala katika mauti.
Se til og svar mig, HERRE min Gud, klar mine Øjne, så jeg ej sover ind i Døden
4 Usimuache adui yangu aseme, “Nimemshinda huyu,” ili kwamba asiweze kusema, “Nimemtawala adui yangu;” la sivyo, maadui zangu watafurahia nitakapo shushwa chini.
og min Fjende skal sige: "Jeg overvandt ham!" mine Uvenner juble, fordi jeg vakler!
5 Lakini nimeamini katika uaminifu wa agano lako; moyo wangu wafurahia katika wokovu wako.
Dog stoler jeg fast på din Miskundhed, lad mit Hjerte juble over din Frelse!
6 Nitamuimbia Yahwe kwa kuwa ameniganga kwa ukarimu kabisa.
Jeg vil synge for HERREN, thi han var mig god!