< Zaburi 129 >
1 “Mara nyingi tangu ujana wangu wamekuwa wakinishambulia,” Israeli na iseme.
Often have they fought against me from my youth, let Israel now say.
2 “Mara nyingi tangu ujana wangu wamekuwa wakinishambulia, lakini hawajanishinda.
Often have they fought against me from my youth: but they could not prevail over me.
3 Wakulima wamekuwa wakilima mgonngoni kwangu; wametengeneza matuta yao marefu.
The wicked have wrought upon my back: they have lengthened their iniquity.
4 Yahwe ni mwenye haki; amezikata kamba za waovu.”
The Lord who is just will cut the necks of sinners:
5 Wote waaibishwe na kurudishwa nyuma, wale wachukiao Sayuni.
Let them all be confounded and turned back that hate Sion.
6 Na wawe kama nyasi juu ya paa ambayo hunyauka kabla hayajakua,
Let them be as grass on the tops of houses: which withered before it be plucked up:
7 ambayo hayawezi kujaza mkono wa mvunaji wala kifua cha mfunga miganda.
Wherewith the mower filleth not his hand: nor he that gathereth sheaves his bosom.
8 Wale wapitao karibu wasiseme, “Baraka za Mungu na ziwe juu yako; Tunakubariki katika jina la Yahwe.”
And they that have passed by have not said: The blessing of the Lord be upon you: we have blessed you in the name of the Lord.