< Zaburi 128 >

1 Amebarikiwa kila mtu amchaye Yahwe, atembeaye katika njia zake.
Wimbo wa kwenda juu. Heri ni wale wote wamchao Bwana, waendao katika njia zake.
2 Kazi ya mikono yako, wewe utaifurahia; utabarikiwa na kufanikiwa.
Utakula matunda ya kazi yako; baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao katika nyumba yako; wanao watakuwa kama miche ya mimea ya mizeituni wakaapo kuzunguka meza yako.
Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao ndani ya nyumba yako; wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni kuizunguka meza yako.
4 Ndiyo, hakika, mtu anaye muheshimu Yahwe atabarikiwa.
Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa mtu amchaye Bwana.
5 Mungu na akubariki toka Sayuni; na uweze kuona mafanikio ya Yerusalemu siku zote za maisha yako.
Bwana na akubariki kutoka Sayuni siku zote za maisha yako, na uone mafanikio ya Yerusalemu,
6 Uishi uwaone wana wa wanao. Amani iwe na Israli.
nawe ujaliwe kuishi uone watoto wa watoto wako. Amani iwe juu ya Israeli.

< Zaburi 128 >