< Zaburi 127 >

1 Yahwe asipoijenga nyumba, waijengao wafanya kazi bure. Yahwe asipoulinda mji, aulindaye afanya kazi bure.
[the] song of The ascents of Solomon if Yahweh - not he will build a house vanity - they have toiled builders its in it if Yahweh not he will watch over a city vanity - he has kept awake [the] watchman.
2 Ni kazi bure kwa wewe unayeamka mapema, na kulala kwa kuchelewa, au kula mkate kwa kuufanyia kazi ngumu, maana Yahwe huwapa chakula awapendao hata wawapo usingizini.
Vanity [belongs] to you - [who] rise early to rise [who] delay to sit [who] eat [the] bread of labors thus he gives to beloved [one] his sleep.
3 Tazama, wana ni urithi kutoka kwa Yahwe, uzao wa tumbo ni thawabu kutoka kwake.
Here! [the] inheritance of Yahweh [is] sons [is] a reward [the] fruit of the womb.
4 Kama mishale mkononi mwa shujaa, ndivyo walivyo wana wa ujanani.
Like arrows in [the] hand of a warrior so [are] [the] sons of youth.
5 Ni namna gani alivyo barikiwa mtu ambaye amelijaza podo lake hivyo. Hata aibishwa pindi atakapo kabiliana na adui zake katika lango.
How blessed! [is] the man who he has filled quiver his from them not they will be ashamed if they will speak with enemies in the gate.

< Zaburi 127 >