< Zaburi 125 >

1 Wale wamwaminio Yahwe ni kama mlima Sayuni, hautikisiki, wadumu milele.
שיר המעלות הבטחים ביהוה כהר ציון לא ימוט לעולם ישב׃
2 Kama milima inavyo izunguka Yerusalemu, hivyo ndivyo Yahwe anavyo wazunguka watu wake sasa na hata milele.
ירושלם הרים סביב לה ויהוה סביב לעמו מעתה ועד עולם׃
3 Fimbo ya uovu haitatawala katika nchi ya wenye haki. Vinginevyo wenye haki wanaweza kukosea.
כי לא ינוח שבט הרשע על גורל הצדיקים למען לא ישלחו הצדיקים בעולתה ידיהם׃
4 Ee Yahwe, utende wema kwa wale walio wema na wale walio wanyoofu mioyoni mwao.
היטיבה יהוה לטובים ולישרים בלבותם׃
5 Lakini kwa wale wanaogeukia njia zao za upotovu, Yahwe atawaondoa pamoja na watenda maovu. Amani iwe na Israeli.
והמטים עקלקלותם יוליכם יהוה את פעלי האון שלום על ישראל׃

< Zaburi 125 >