< Zaburi 125 >
1 Wale wamwaminio Yahwe ni kama mlima Sayuni, hautikisiki, wadumu milele.
A Song of Ascents. They that trust in the LORD are as mount Zion, which cannot be moved, but abideth for ever.
2 Kama milima inavyo izunguka Yerusalemu, hivyo ndivyo Yahwe anavyo wazunguka watu wake sasa na hata milele.
As the mountains are round about Jerusalem, so the LORD is round about his people, from this time forth and for evermore.
3 Fimbo ya uovu haitatawala katika nchi ya wenye haki. Vinginevyo wenye haki wanaweza kukosea.
For the sceptre of wickedness shall not rest upon the lot of the righteous; that the righteous put not forth their hands unto iniquity.
4 Ee Yahwe, utende wema kwa wale walio wema na wale walio wanyoofu mioyoni mwao.
Do good, O LORD, unto those that be good, and to them that are upright in their hearts.
5 Lakini kwa wale wanaogeukia njia zao za upotovu, Yahwe atawaondoa pamoja na watenda maovu. Amani iwe na Israeli.
But as for such as turn aside unto their crooked ways, the LORD shall lead them forth with the workers of iniquity. Peace be upon Israel.