< Zaburi 125 >

1 Wale wamwaminio Yahwe ni kama mlima Sayuni, hautikisiki, wadumu milele.
They that trust in the Lord shall be as mount Sion: he shall not be moved for ever that dwelleth
2 Kama milima inavyo izunguka Yerusalemu, hivyo ndivyo Yahwe anavyo wazunguka watu wake sasa na hata milele.
In Jerusalem. Mountains are round about it: so the Lord is round about his people from henceforth now and for ever.
3 Fimbo ya uovu haitatawala katika nchi ya wenye haki. Vinginevyo wenye haki wanaweza kukosea.
For the Lord will not leave the rod of sinners upon the lot of the just: that the just may not stretch forth their hands to iniquity.
4 Ee Yahwe, utende wema kwa wale walio wema na wale walio wanyoofu mioyoni mwao.
Do good, O Lord, to those that are good, and to the upright of heart.
5 Lakini kwa wale wanaogeukia njia zao za upotovu, Yahwe atawaondoa pamoja na watenda maovu. Amani iwe na Israeli.
But such as turn aside into bonds, the Lord shall lead out with the workers of iniquity: peace upon Israel.

< Zaburi 125 >