< Zaburi 124 >
1 “Kama Yahwe asingekuwa upande wetu,” Israeli na aseme sasa,
A song of ascents. Of David. “Had it not been the Lord who was for us” let Israel say
2 “Kama asingekuwa Yahwe ambaye alikuwa upande wetu wakati watu walipoinuka dhidi yetu,
“Had it not been the Lord who was for us when enemies rose against us,
3 basi wangekuwa wametumeza tungali hai hasira yao lipozidi dhidi yetu.
then alive they’d have swallowed us up, when their anger was kindled against us.
4 Maji yangetugharikisha; mto ungetuzidia.
Then the waters would’ve swept us away, and the torrent passed over us clean:
5 Kisha maji yafurikayo yangetuzamisha.”
then most sure would’ve passed over us clean the wild seething waters.”
6 Atukuzwe Yahwe, ambaye hajaruhusu tuwe mawindo kwa meno yao.
Blest be the Lord who has given us not to be torn by their teeth.
7 Tumetoroka kama ndege mtegoni mwa wawindaji; mtego umevunjika, nasi tumetoroka.
We are like a bird just escaped from the snare of the fowler. The snare is broken, and we are escaped.
8 Msaada wetu uko katika Yahwe, aliyeziumba mbingu na nchi.
Our help is the name of the Lord, the Creator of heaven and earth.