< Zaburi 124 >
1 “Kama Yahwe asingekuwa upande wetu,” Israeli na aseme sasa,
A Song of Ascents; of David. 'If it had not been the LORD who was for us', let Israel now say;
2 “Kama asingekuwa Yahwe ambaye alikuwa upande wetu wakati watu walipoinuka dhidi yetu,
'If it had not been the LORD who was for us, when men rose up against us,
3 basi wangekuwa wametumeza tungali hai hasira yao lipozidi dhidi yetu.
Then they had swallowed us up alive, when their wrath was kindled against us;
4 Maji yangetugharikisha; mto ungetuzidia.
Then the waters had overwhelmed us, the stream had gone over our soul;
5 Kisha maji yafurikayo yangetuzamisha.”
Then the proud waters had gone over our soul.'
6 Atukuzwe Yahwe, ambaye hajaruhusu tuwe mawindo kwa meno yao.
Blessed be the LORD, who hath not given us as a prey to their teeth.
7 Tumetoroka kama ndege mtegoni mwa wawindaji; mtego umevunjika, nasi tumetoroka.
Our soul is escaped as a bird out of the snare of the fowlers; the snare is broken, and we are escaped.
8 Msaada wetu uko katika Yahwe, aliyeziumba mbingu na nchi.
Our help is in the name of the LORD, who made heaven and earth.