< Zaburi 122 >

1 Nilifurahi waliponiambia, “Na twende kwenye Nyumba ya Yahwe.”
שיר המעלות לדוד שמחתי באמרים לי-- בית יהוה נלך
2 Ee Yerusalemu, miguu yetu imesimama ndani ya malango yako!
עמדות היו רגלינו-- בשעריך ירושלם
3 Ee Yerusalemu, uliojengwa kama mji uliopangiliwa kwa umakini!
ירושלם הבנויה-- כעיר שחברה-לה יחדו
4 Makabila huenda juu Yerusalemu, makabila ya Yahwe; kama ushuhuda wa Israeli, kulishukuru jina la Yahwe.
ששם עלו שבטים שבטי-יה--עדות לישראל להדות לשם יהוה
5 Huko viliwekwa viti vya hukumu, viti vya enzi vya nyumba ya Daudi.
כי שמה ישבו כסאות למשפט כסאות לבית דוד
6 Ombeni kwa ajili ya amani ya Yerusalemu! “Wote wakupendao wawe na amani.
שאלו שלום ירושלם ישליו אהביך
7 Amani iwepo ndani ya kuta zako ili ikutetee, na wawe na amani ndani ya ngome zako.”
יהי-שלום בחילך שלוה בארמנותיך
8 Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu nitasema, “Amani iwe ndani yenu.”
למען אחי ורעי-- אדברה-נא שלום בך
9 Kwa ajili ya Yahwe Mungu wetu, nitatafuta mema kwa ajili yako.
למען בית-יהוה אלהינו-- אבקשה טוב לך

< Zaburi 122 >