< Zaburi 121 >

1 Nitayainua macho yangu nitazame milimani. Msaada wangu utatoka wapi?
تَرْنِيمَةُ الْمَصَاعِدِ أَرْفَعُ عَيْنَيَّ إِلَى الْجِبَالِ. مِنْ أَيْنَ يَأْتِي عَوْنِي؟١
2 Msaada wangu unatoka kwa Yahwe, aliyezifanya mbingu na nchi.
يَأْتِي عَوْنِي مِنْ عِنْدِ الرَّبِّ، صَانِعِ السَّمَاوَاتِ وَالأَرْضِ.٢
3 Hatauacha mguu wako uteleze; yeye akulindaye hatasinzia.
لَا يَدَعُ قَدَمَكَ تَزِلُّ. لَا يَنْعَسُ حَافِظُكَ.٣
4 Tazama, mlinzi wa Israeli hatasinzia wala hatalala usingizi kamwe.
لَا يَنْعَسُ وَلَا يَنَامُ حَافِظُ إِسْرَائِيلَ.٤
5 Yahwe ni mlinzi wako; Yahwe ni uvuli mkono wako wa kuume.
الرَّبُّ هُوَ حَافِظُكَ، الرَّبُّ سِتْرٌ لَكَ عَنْ يَمِينِكَ.٥
6 Jua halitakudhuru wakati wa mchana, wala mwezi wakati wa usiku.
لَنْ تَضْرِبَكَ الشَّمْسُ بِحَرِّهَا نَهَاراً وَلَا الْقَمَرُ بِنُورِهِ لَيْلاً.٦
7 Yahwe atakulinda na madhara yote, na ataulinda uhai wako.
يَقِيكَ الرَّبُّ مِنْ كُلِّ شَرٍّ. يَقِي نَفْسَكَ.٧
8 Yahwe atakulinda katika yote ufanyayo sasa na hata milele.
الرَّبُّ يَحْفَظُ ذِهَابَكَ وَإِيَابَكَ مِنَ الآنَ وَإِلَى الأَبَدِ.٨

< Zaburi 121 >