< Zaburi 120 >

1 Katika dhiki yangu nilimuita Yahwe, naye akanijibu.
Wimbo wa kwenda juu. Katika dhiki yangu namwita Bwana, naye hunijibu.
2 Uiokoe nasfi yangu, yahwe, dhidi ya wale wadanganyao kwa midomo yao na wanenao hila kwa ndimi zao.
Ee Bwana, uniokoe kutoka midomo ya uongo na ndimi za udanganyifu.
3 Yahwe atawaadhibu vipi, na atawafanyia kitu gani zaidi, ninyi mlio na ulimi mdanganyifu?
Atakufanyia nini, au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?
4 Atawaadhibu kwa mishale ya shujaa iliyo nolewa kwa makaa ya moto ya mretemu.
Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa, kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.
5 Ole wangu mimi kwa sababu ninaishi kwa muda Mesheki; huko nyuma niliishi kati ya maskani ya Kedari.
Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki, kwamba naishi katikati ya hema za Kedari!
6 Kwa muda mrefu sana niliisha na wale waichukiao amani.
Nimeishi muda mrefu mno miongoni mwa wale wanaochukia amani.
7 Nipo kwa ajili ya amani, lakini ninenapo, wao wako kwa ajili ya vita.
Mimi ni mtu wa amani; lakini ninaposema, wao wanataka vita.

< Zaburi 120 >