< Zaburi 120 >
1 Katika dhiki yangu nilimuita Yahwe, naye akanijibu.
Canticum graduum. [Ad Dominum cum tribularer clamavi, et exaudivit me.
2 Uiokoe nasfi yangu, yahwe, dhidi ya wale wadanganyao kwa midomo yao na wanenao hila kwa ndimi zao.
Domine, libera animam meam a labiis iniquis et a lingua dolosa.
3 Yahwe atawaadhibu vipi, na atawafanyia kitu gani zaidi, ninyi mlio na ulimi mdanganyifu?
Quid detur tibi, aut quid apponatur tibi ad linguam dolosam?
4 Atawaadhibu kwa mishale ya shujaa iliyo nolewa kwa makaa ya moto ya mretemu.
Sagittæ potentis acutæ, cum carbonibus desolatoriis.
5 Ole wangu mimi kwa sababu ninaishi kwa muda Mesheki; huko nyuma niliishi kati ya maskani ya Kedari.
Heu mihi, quia incolatus meus prolongatus est! habitavi cum habitantibus Cedar;
6 Kwa muda mrefu sana niliisha na wale waichukiao amani.
multum incola fuit anima mea.
7 Nipo kwa ajili ya amani, lakini ninenapo, wao wako kwa ajili ya vita.
Cum his qui oderunt pacem eram pacificus; cum loquebar illis, impugnabant me gratis.]