< Zaburi 120 >
1 Katika dhiki yangu nilimuita Yahwe, naye akanijibu.
When I had troubles, I called out to Yahweh and he answered me.
2 Uiokoe nasfi yangu, yahwe, dhidi ya wale wadanganyao kwa midomo yao na wanenao hila kwa ndimi zao.
[I prayed], “Yahweh, rescue/save me from people [SYN, MTY] who lie to me and [try to] deceive me!”
3 Yahwe atawaadhibu vipi, na atawafanyia kitu gani zaidi, ninyi mlio na ulimi mdanganyifu?
You people who lie to me, [I will tell you] [RHQ] what [God] will do to you and what he will do to punish you.
4 Atawaadhibu kwa mishale ya shujaa iliyo nolewa kwa makaa ya moto ya mretemu.
He will shoot sharp arrows at you like soldiers do, and he will [burn you with] red-hot coals from [the wood of] a broom tree.
5 Ole wangu mimi kwa sababu ninaishi kwa muda Mesheki; huko nyuma niliishi kati ya maskani ya Kedari.
It is terrible for me, living among cruel/savage [DOU] people [like those who live] in Meshech [region] and Kedar [region].
6 Kwa muda mrefu sana niliisha na wale waichukiao amani.
I have lived for a long time among people who hate [to live with others] peacefully.
7 Nipo kwa ajili ya amani, lakini ninenapo, wao wako kwa ajili ya vita.
Every time I talk about living together peacefully, they talk about starting a war.