< Zaburi 12 >

1 Msaada, Yahweh, kwa kuwa wacha Mungu wametoweka; nao waaminifu wametokomea.
TO THE OVERSEER. ON THE EIGHTH. A PSALM OF DAVID. Save, YHWH, for the saintly has failed, For the steadfast have ceased From the sons of men:
2 Kila mmoja anasema kwa jirani yake maneno matupu; kila mmoja anaongea kwa midomo yenye sifa za uongo na maneno ya udanganyifu.
They each speak vanity with his neighbor, Lip of flattery! With heart and heart they speak.
3 Yahweh, katilia mbali midomo yenye sifa za uongo, kila ulimi unanena kwa nguvu mambo makubwa.
YHWH cuts off all lips of flattery, A tongue speaking great things,
4 Hawa ni wale ambao wamesema, “Kwa ndimi zetu tutashinda. Wakati midomo yetu itakapo ongea, ni nani atakaye kuwa mtawala juu yetu?”
Who said, “By our tongue we do mightily: Our lips [are] our own; who [is] lord over us?”
5 “Kwa sababu ya vurugu zilizopo kinyume na maskini, na kwa sababu ya kuugua kwao wahitaji, Nitainuka,” asema Yahwe. “Nitawaletea usalama wanao hitaji.”
Because of the spoiling of the poor, Because of the groaning of the needy, Now I arise, says YHWH, I set in safety [him who] breathes for it.
6 Maneno ya Yahwe ni masafi, kama fedha iliyo safishwa katika tanuru duniani, iliyo ng'arishwa mara saba zaidi.
Sayings of YHWH [are] pure sayings—Silver tried in a furnace of earth, refined sevenfold.
7 Wewe ni Yahwe! Unaye watunza. Una wahifadhi wacha Mungu kutoka katika hiki kizazi cha waovu na hata milele.
You, O YHWH, preserve them, You keep us from this generation for all time.
8 Waovu hutembea kila pande pale uovu unapoinuliwa kati ya wanadamu.
The wicked walk around continually, According as vileness is exalted by sons of men!

< Zaburi 12 >