< Zaburi 119 >
1 Wamebarikiwa wale ambao njia zao hazina lawama, waenendao katika sheria ya Yahwe.
Heri wale walio waadilifu katika njia zao, wanaoenenda katika sheria ya Bwana.
2 Wamebarikiwa wale wazishikao amri zake thabiti, wamtafutao kwa moyo wao wote.
Heri wale wanaozishika shuhuda zake, wamtafutao kwa moyo wao wote.
3 Hawatendi makosa; wanaenenda katika njia zake.
Wasiofanya lolote lililo baya, wanaoenenda katika njia zake.
4 Wewe umetuamuru kuyashika maagizo yako ili tuyachunguze kwa umakini.
Umetoa maagizo yako ili tuyatii kwa ukamilifu.
5 Oh, ningependa njia zangu ziwe thabiti nizitii amri zako!
Laiti mwenendo wangu ungekuwa imara katika kuyatii maagizo yako!
6 Ndipo sitaaibika nizifikiripo amri zako zote.
Hivyo mimi sitaaibishwa ninapozingatia amri zako zote.
7 Nitakushukuru wewe kwa unyofu wangu wa moyo nijifunzapo amri za haki yako.
Nitakusifu kwa moyo mnyofu ninapojifunza sheria zako za haki.
8 Nitazitii amri zako; usiniache peke yangu. BETH.
Nitayatii maagizo yako; usiniache kabisa.
9 Ni jinsi gani kijana aweza kuendelea kuishi katika njia yake ya utakatifu? Ni kwa kulitii neno lako.
Kijana aifanye njia yake kuwa safi jinsi gani? Ni kwa kutii, akilifuata neno lako.
10 Kwa moyo wangu wote ninakutafuta wewe; Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.
Ninakutafuta kwa moyo wangu wote, usiniache niende mbali na amri zako.
11 Moyoni mwangu nimeliweka neno lako ili nisije nikakutenda dhambi.
Nimelificha neno lako moyoni mwangu ili nisikutende dhambi.
12 Umetukuka, Yahwe; unifundishe amri zako.
Sifa ni zako, Ee Bwana, nifundishe maagizo yako.
13 Kwa kinywa changu nimetangaza amri ya haki yako yote ambayo umeifunua.
Kwa midomo yangu nitasimulia sheria zote zinazotoka katika kinywa chako.
14 Ninafurahi katika njia ya amri za agano lako zaidi kuliko katika utajiri.
Ninafurahia kufuata sheria zako kama mtu afurahiaye mali nyingi.
15 Nitayatafakari maagizo yako na kuzitilia maanani njia zako.
Ninatafakari maagizo yako na kuziangalia njia zako.
16 Ninafurahia katika amri zako; sitalisahau neno lako. GIMEL.
Ninafurahia maagizo yako, wala sitalipuuza neno lako.
17 Uwe mwema kwa mtumishi wako ili niweze kuishi na kulishika neno lako.
Mtendee mema mtumishi wako, nami nitaishi; nitalitii neno lako.
18 Ufungue macho yangu ili niweze kuona mambo ya ajabu katika sheria yako.
Yafungue macho yangu nipate kuona mambo ya ajabu katika sheria yako.
19 Mimi ni mgeni katika nchi; usizifiche amri zako mbali nami.
Mimi ni mgeni duniani, usinifiche amri zako.
20 Moyo wangu unauma kwa kutamani sana kuzijua amri zako za haki wakati wote.
Nafsi yangu inataabika kwa shauku kubwa juu ya sheria zako wakati wote.
21 Wewe huwakemea wenye kiburi, waliolaaniwa, wanao tanga-tanga mbali na amri zako.
Unawakemea wenye majivuno, waliolaaniwa waendao mbali na amri zako.
22 Uniokoe dhidi ya aibu na udhalilishaji, maana nimezitii amri za agano lako.
Niondolee dharau na dhihaka, kwa kuwa ninazishika sheria zako.
23 Ingawa watawala wanapanga njama na kunikashfu, mtumishi wako huzitafakali amri zako.
Ingawa watawala huketi pamoja na kunisingizia, mtumishi wako atatafakari juu ya maagizo yako.
24 Amri za agano lako ni furaha yangu, na washauri wangu. DALETH.
Sheria zako ni furaha yangu, nazo ni washauri wangu.
25 Uhai wangu unashikamana na mavumbi! nipe uhai kwa neno lako.
Nimelazwa chini mavumbini, yahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.
26 Nilikuambia mapito yangu, na ulinijibu; nifundishe sheria zako.
Nilikueleza njia zangu ukanijibu, nifundishe sheria zako.
27 Unifahamishe njia ya maagizo yako, ili niweze kutafakari juu ya mafundisho yako ya ajabu.
Nijulishe mafundisho ya mausia yako, nami nitatafakari maajabu yako.
28 Nimelemewa na huzuni! Nitie nguvu kwa neno lako.
Nafsi yangu imechakazwa kwa huzuni, uniimarishe sawasawa na neno lako.
29 Uiondoe kwangu njia ya udanganyifu; kwa wema wako unifundishe sheria yako.
Niepushe na njia za udanganyifu, kwa neema unifundishe sheria zako.
30 Nimechagua njia ya uaminifu; siku zote nimeweka amri za haki yako mbele yangu.
Nimechagua njia ya kweli, nimekaza moyo wangu katika sheria zako.
31 Ninashikamana na amri za agano lako; Yahwe, usiniache niaibike.
Nimengʼangʼania sheria zako, Ee Bwana, usiniache niaibishwe.
32 Nitakimbia katika njia ya amri zako, kwa sababu wausukuma moyo wangu kufanya hivyo. HE
Nakimbilia katika njia ya maagizo yako, kwa kuwa umeuweka moyo wangu huru.
33 Unifundishe, Yahwe, njia za sheria yako, nami nitazishika hadi mwisho.
Ee Bwana, nifundishe kuyafuata maagizo yako, nami nitayashika mpaka mwisho.
34 Unipe uelewa, nami nitazishika sheria zako; nitazitii kwa moyo wangu wote.
Nipe ufahamu, nami nitaishika sheria yako na kuitii kwa moyo wangu wote.
35 Uniongoze katika njia ya amri zako, maana ninafurahi kuenenda katika hizo.
Niongoze kwenye njia ya amri zako, kwa kuwa huko napata furaha.
36 Uelekeze moyo wangu kuzielekea amari za agano lako na uniweke mbali na matendo yasiyo haki tena.
Ugeuze moyo wangu kuelekea sheria zako, na siyo kwenye mambo ya ubinafsi.
37 Uyageuze macho yangu dhidi ya kutazama mambo yasiyofaa; unihuishe katika njia zako.
Geuza macho yangu kutoka kwenye mambo yasiyofaa, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na neno lako.
38 Umtendee mtumishi wako ahadi ambayo uliifanya kwa wale wanaokuheshimu wewe.
Mtimizie mtumishi wako ahadi yako, ili upate kuogopwa.
39 Uniondolee shutumu niiogopayo, maana hukumu zako za haki ni njema.
Niondolee aibu ninayoiogopa, kwa kuwa sheria zako ni njema.
40 Tazama, nimeyatamani maagizo yako; unihuishe katika haki yako. VAV.
Tazama jinsi ninavyoonea shauku mausia yako! Hifadhi maisha yangu katika haki yako.
41 Ee Yahwe, unipe upendo wako usiokwisha na wokovu wako kulingana na ahadi yako;
Ee Bwana, upendo wako usiokoma unijie, wokovu wako sawasawa na ahadi yako,
42 ndipo nitakuwa na jibu kwa ajili ya yule anayenidhihaki.
ndipo nitakapomjibu anayenidhihaki, kwa kuwa ninalitumainia neno lako.
43 Usiliondoe neno la kweli mdomoni mwangu, maana nimesubiri kwa ajili ya amri zako za haki.
Usilinyakue neno la kweli kutoka kinywani mwangu, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika amri zako.
44 Nitazitii sheria zako siku zote, milele na milele.
Nitaitii amri yako daima, naam, milele na milele.
45 Nitaenenda salama, maana ninayatafuta maagizo yako.
Nitatembea nikiwa huru, kwa kuwa nimejifunza mausia yako.
46 Nitazinena amri zako thabiti mbele ya wafalme nami sitaaibika.
Nitasema sheria zako mbele za wafalme wala sitaaibishwa,
47 Ninafurahia katika amri zako, nizipendazo sana.
kwa kuwa ninazifurahia amri zako kwa sababu ninazipenda.
48 Nitaziinulia mikono yangu amri zako, nizipendazo; nitazitafakari sheria zako. ZAYIN.
Ninaziinulia amri zako ambazo ninazipenda mikono yangu, nami ninatafakari juu ya maagizo yako.
49 Kumbuka ahadi yako kwa mtumishi wako kwa sababu umenipa tumaini.
Kumbuka neno lako kwa mtumishi wako, kwa sababu umenipa tumaini.
50 Hii ni faraja yangu katika mateso: kuwa ahadi yako imeniweka hai.
Faraja yangu katika mateso yangu ni hii: Ahadi yako inahifadhi maisha yangu.
51 Wenye kiburi wamenicheka, lakini sijaiacha sheria yako.
Wenye majivuno wamenisimanga bila kuchoka, hata hivyo sitaiacha sheria yako.
52 Nimezitafakari amri zako za haki tangu zamani, Yahwe, nami ninajifariji mwenyewe.
Ee Bwana, ninazikumbuka sheria zako za zamani, nazo zinanifariji.
53 Hasira kali imenishikilia kwa sababu ya waovu wanaoikataa sheria yako.
Nimeshikwa sana na ghadhabu kwa ajili ya waovu, ambao wameacha sheria yako.
54 Sheria zako zimekuwa nyimbo zangu katika nyumba ninayoishi kwa muda.
Maagizo yako ni kiini cha nyimbo zangu popote ninapoishi.
55 Ninalifikiria jina lako wakati wa usiku, Yahwe, na kuzishika sheria zako.
Ee Bwana, wakati wa usiku ninalikumbuka jina lako, nami nitatii sheria yako.
56 Hili limekuwa zoezi langu kwa sababu nimeyatii maagizo yako. HETH.
Hili limekuwa zoezi langu: nami ninayatii mausia yako.
57 Yahwe ni sehemu yangu; nimeamua kuyatii maneno yake.
Ee Bwana, wewe ni fungu langu, nimeahidi kuyatii maneno yako.
58 Kwa bidii ninaomba neema yako kwa moyo wangu wote; unihurumie, kama neno lako lilivyo ahidi.
Nimetafuta uso wako kwa moyo wangu wote, nihurumie sawasawa na ahadi yako.
59 Nilizichunguza njia zangu na kugeuzia miguu yangu kwenye amri za agano lako.
Nimezifikiri njia zangu na nimeelekeza hatua zangu katika mausia yako.
60 Naharakisha na sichelewi kuzishika amri zako.
Nitafanya haraka bila kuchelewa kuzitii amri zako.
61 Kamba za waovu zimenifunga; nami sijaisahau sheria yako.
Hata waovu wanifunge kwa kamba, sitasahau sheria yako.
62 Katikati ya usiku ninaamka kukushukuru wewe kwa sababu ya amri za haki yako.
Usiku wa manane ninaamka kukushukuru kwa sababu ya sheria zako za haki.
63 Ninaurafiki na wale wanao kuabudu wewe, wale wote watiio maagizo yako.
Mimi ni rafiki kwa wale wote wakuchao, kwa wote wanaofuata mausia yako.
64 Yahwe, nchi, imejaa uaminifu wa agano lako; unifundishe sheria zako. TETH.
Ee Bwana, dunia imejaa upendo wako, nifundishe maagizo yako.
65 Wewe umemtendea mema mtumishi wako, Yahwe, sawasawa na neno lako.
Mtendee wema mtumishi wako Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
66 Unifundishe utambuzi sahihi na uelewa, kwa kuwa nimeamini katika amri zako.
Nifundishe maarifa na uamuzi mzuri, kwa kuwa ninaamini amri zako.
67 Kabla sijateswa nilipotea, lakini sasa nimelitii neno lako.
Kabla sijapata shida nilipotea njia, lakini sasa ninalitii neno lako.
68 Wewe ni mwema, na ndiye yule utendaye mema; unifundishe sheria zako.
Wewe ni mwema, unalotenda ni jema, nifundishe maagizo yako.
69 Wenye kiburi wamenichafua kwa uongo, lakini niliyashika maagizo yako kwa moyo wangu wote.
Ingawa wenye majivuno wamenisingizia uongo, nitafuata mausia yako kwa moyo wangu wote.
70 Mioyo yao ni migumu, lakini ninafurahia katika sheria yako.
Mioyo yao ni katili na migumu, bali mimi napendezwa na sheria yako.
71 Ni vizuri kwangu kuwa nimeteseka ili niweze kujifunza sheria zako.
Ilikuwa vyema mimi kupata shida ili nipate kujifunza maagizo yako.
72 Maagizo yatokayo kinywani mwako ni ya thamani zaidi kwangu kuliko maelfu ya vipande vya dhahabu na fedha. YOD.
Sheria inayotoka kinywani mwako ina thamani kubwa kwangu kuliko maelfu ya vipande vya fedha na dhahabu.
73 Mikono yako imeniumba na kunitengeneza; unipe uelewa ili niweze kujifunza amri zako.
Mikono yako ilinifanya na kuniumba, nipe ufahamu niweze kujifunza amri zako.
74 Wale wanao kucha wewe watafurahi wanionapo kwa sababu ninapata tumaini katika neno lako.
Wakuchao wafurahie wanaponiona, kwa kuwa nimeweka tumaini langu katika neno lako.
75 Ninajua, Yahwe, kuwa amri zako ni za haki, na kuwa katika uaminifu ulinitesa.
Ee Bwana, ninajua kwamba sheria zako ni za haki, katika uaminifu wako umeniadhibu.
76 Agano lako aminifu na linifariji, kama ulivyomwahidi mtumishi wako.
Upendo wako usiokoma uwe faraja yangu, sawasawa na ahadi yako kwa mtumishi wako.
77 Unihurumie ili niweze kuishi, kwa maana sheria yako ni furaha yangu.
Huruma yako na inijie ili nipate kuishi, kwa kuwa naifurahia sheria yako.
78 Wenye kiburi na waaibishwe, maana wamenitukana; bali mimi nitayatafakari maagizo yako.
Wenye majivuno na waaibishwe kwa kunikosea mimi bila sababu, lakini mimi nitatafakari juu ya mausia yako.
79 Wale wote wanao kucha wewe na wanigeukie, wale wazijuao amri za agano lako.
Wale wakuchao na wanigeukie mimi, hao ambao wanazielewa sheria zako.
80 Moyo wangu uwe mkamilifu pamoja na heshima kwa sheria zako ili nisiaibike. KAPH.
Moyo wangu usiwe na lawama katika kutii maagizo yako, ili nisiaibishwe.
81 Ninazimia kwa kutamani sana kuwa wewe unaweza kuniokoa! Ninamatumaini katika neno lako.
Nafsi yangu inazimia kwa kutamani wokovu wako, lakini nimeweka tumaini langu katika neno lako.
82 Macho yangu yanatamani sana kuiona ahadi yako; ni lini utanifariji mimi?
Macho yangu yamefifia, nikingoja ahadi yako; ninasema, “Utanifajiri lini?”
83 Kwa maana nimekuwa kama kiriba katika moshi; sisahau sheria zako.
Ingawa nimekuwa kama kiriba kwenye moshi, bado sijasahau maagizo yako.
84 Ni kwa muda gani gani mtumishi wako atalazimika kuyavumilia haya; ni lini utawahukumu wale wanaonitesa?
Mtumishi wako itampasa angoje mpaka lini? Ni lini utawaadhibu washtaki wangu?
85 Wenye kiburi wamenichimbia shimo, wasiotii sheria yako.
Wenye majivuno wananichimbia mashimo, kinyume na sheria yako.
86 Amri zako zote ni za kuaminika; wale watu walinitesa bila ya haki; unisaidie.
Amri zako zote ni za kuaminika; unisaidie, kwa sababu watu wananishtaki bila sababu.
87 karibu kunifanya nifikie mwisho juu ya nchi hii, lakini siyakatai maagizo yako.
Walikaribia kabisa kunifuta kutoka uso wa dunia, lakini sijaacha mausia yako.
88 Kwa upendo wako thabiti, uniweke hai, ili niweze kuzitii amri zako. LAMEDH.
Yahifadhi maisha yangu sawasawa na upendo wako, nami nitatii sheria za kinywa chako.
89 Yahwe, neno lako linasimama milele; neno lako limefanywa imara mbinguni.
Ee Bwana, neno lako ni la milele, linasimama imara mbinguni.
90 Uaminifu wako wadumu kwa ajili ya vizazi vyote; umeiimarisha nchi, nayo inadumu.
Uaminifu wako unaendelea kwa vizazi vyote, umeiumba dunia, nayo inadumu.
91 Vitu yote yaliendelea mpaka leo hii, kama vile ulivyosema katika amri zako za haki, maana vitu vyote ni watumishi wako.
Sheria zako zinadumu hadi leo, kwa kuwa vitu vyote vinakutumikia.
92 Kama sheria yako isingekuwa furaha yangu, ningeangamia katika mateso yangu.
Kama nisingefurahia sheria yako, ningeangamia katika taabu zangu.
93 Sitayasahau kamwe maagizo yako, maana kupitia hayo umeniweka hai.
Sitasahau mausia yako kamwe, kwa maana kwayo umehifadhi maisha yangu.
94 Mimi ni wako, kwa maana ninayatafuta maagizo yao.
Uniokoe, kwa maana mimi ni wako, kwa kuwa nimetafuta mausia yako.
95 Waovu hujiandaa kuniangamiza, lakini nitatafuta kuzielewa amri za agano lako.
Waovu wanangojea kuniangamiza, bali mimi ninatafakari sheria zako.
96 Nimeona kuwa kila kitu kina mipaka, lakini amri zako ni pana, zaidi ya mipaka. MEM.
Katika ukamilifu wote ninaona mna kikomo, lakini amri zako hazina mpaka.
97 Oh ni jinsi gani naipenda sheria yako! Ni tafakari yangu mchana kutwa.
Aha! Tazama, sheria yako naipenda mno ajabu. Ninaitafakari mchana kutwa.
98 Amri zako hunifanya mwenye hekima kuliko adui zangu, maana amri zako siku zote ziko pamoja nami.
Amri zako zimenipa hekima zaidi kuliko adui zangu, kwa kuwa nimezishika daima.
99 Ninauelewa zaidi kuliko walimu wangu wote, kwa maana ninazitafakari amri za agano lako.
Nina akili zaidi kuliko walimu wangu wote, kwa kuwa ninatafakari juu ya sheria zako.
100 Ninaelewa kuliko wale wanaonizidi umri; hii ni kwa sababu nimeyashika maagizo yako.
Nina ufahamu zaidi kuliko wazee, kwa kuwa ninayatii mausia yako.
101 Nimeiepusha miguu yangu na kila njia ya uovu ili niweze kulitii neno lako.
Nimezuia miguu yangu isiende kwenye kila njia mbaya, ili niweze kutii neno lako.
102 Sijaenda kinyume na amri zako za haki, kwa maana wewe umenifundisha.
Sijaziacha sheria zako, kwa kuwa umenifundisha wewe mwenyewe.
103 Ni jinsi gani maneno yako ni matamu kwenye majaribu yangu, naam, matamu kuliko asali kinywani mwangu!
Tazama jinsi maneno yako yalivyo matamu kwangu, matamu kuliko asali katika kinywa changu!
104 Kupitia maagizo yako ninapata utambuzi; kwa hiyo kila njia isiyo ya kweli.
Ninapata ufahamu kutoka mausia yako, kwa hiyo ninachukia kila njia ya upotovu.
105 Neno lako ni taa ya mguu miguu yangu na mwanga wa njia yangu.
Neno lako ni taa ya miguu yangu na mwanga katika njia yangu.
106 Nimeapa na nimethibitisha, kuwa nitazitii amri za haki yako.
Nimeapa na nimethibitisha, kwamba nitafuata sheria zako za haki.
107 Nimeteswa sana; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika neno lako.
Nimeteseka sana, uhifadhi maisha yangu, Ee Bwana, sawasawa na neno lako.
108 Yahwe, tafadhali pokea dhabihu yangu ya hiari ya kinywa changu, na unifundishe amri zako za haki.
Ee Bwana, pokea sifa za hiari za kinywa changu, nifundishe sheria zako.
109 Uhai wangu ziku zote uko mkononi mwangu, lakini bado sisahau sheria yako.
Ingawa maisha yangu yako hatarini siku zote, sitasahau sheria yako.
110 Waovu wamenitegea mtego, lakini sijapotea mbali na maagizo yako.
Waovu wamenitegea mtego, lakini sijayakiuka maagizo yako.
111 Nimezifanya amri za agano lako kama urithi wangu milele, maana hizo ni furaha ya moyo wangu.
Sheria zako ni urithi wangu milele, naam ni furaha ya moyo wangu.
112 Moyo wangu umewekwa kuzitii sheria zako milele mpaka mwisho kabisa. SAMEKH.
Nimekusudia moyoni mwangu kuyafuata maagizo yako mpaka mwisho.
113 Ninawachukia watu wa kusita-sita, lakini naipenda sheria yako.
Ninachukia watu wa nia mbili, lakini ninapenda sheria yako.
114 Wewe ni ficho langu na ngao yangu; nalingoja neno lako.
Wewe ni kimbilio langu na ngao yangu, nimeweka tumaini langu katika neno lako.
115 Ondokeni kwangu, ninyi mtendao uovu, ili niweze kuzitii amri za Mungu wangu.
Ondokeni kwangu, ninyi mtendao mabaya, ili niweze kushika amri za Mungu wangu!
116 Uniwezeshe kwa neno lako ili niweze kuishi na nisiaibike na matumaini yangu.
Nihifadhi sawasawa na ahadi yako, nami nitaishi; usiache matumaini yangu yakavunjwa.
117 Unisaidie, nami nitakuwa salama; siki zote nitazitafakari sheria zako.
Nitegemeze, nami nitaokolewa, nami daima nitayaheshimu maagizo yako.
118 Wewe huwakataa wale wote wapoteao mbali na sheria zako, maana watu hao ni wadanganyifu na si wakuaminika.
Unawakataa wote wanaoyaasi maagizo yako, kwa maana udanganyifu wao ni bure.
119 Wewe huwaondoa waovu wa nchi kama takataka; kwa hiyo ninazipenda amri zako thabiti.
Waovu wa nchi unawatupa kama takataka, kwa hivyo nazipenda sheria zako.
120 Mwili wangu hutetemeka kwa hofu yako, na ninaziogopa amri za haki yako. AYIN.
Mwili wangu unatetemeka kwa kukuogopa wewe, ninaziogopa sheria zako.
121 Ninafanya kilicho sahihi na haki; usiniache kwa watesi wangu.
Nimetenda yaliyo haki na sawa, usiniache mikononi mwa watesi wangu.
122 Uwe mdhamini wa ustawi wa mtumishi wako; usiwaache wenye kiburi wanionee.
Mhakikishie mtumishi wako usalama, usiache wenye kiburi wanionee.
123 Macho yangu yanachoka kwa kuusubiri wokovu wako na neno lako la haki.
Macho yangu yamefifia, yakitazamia wokovu wako, na kuitazamia ahadi yako ya kweli.
124 Mwoneshe mtumishi wako uaminifu wa agano lako, na unifundishe sheria zako.
Mfanyie mtumishi wako kulingana na upendo wako na unifundishe maagizo yako.
125 Mimi ni mtumishi wako; unipe uelewa ili niweze kuzijua amri za agano lako.
Mimi ni mtumishi wako; nipe ufahamu ili niweze kuelewa sheria zako.
126 Ni wakati wa Yahwe kutenda, kwa maana watu wamevunja sheria yako.
Ee Bwana, wakati wako wa kutenda umewadia, kwa kuwa sheria yako inavunjwa.
127 Hakika ninazipenda amri zako kuliko dhahabu, naam, kuliko dhahabu safi.
Kwa sababu nazipenda amri zako zaidi ya dhahabu, naam, zaidi ya dhahabu safi,
128 Hivyo ninayafuata maagizo yako yote kwa makini, na ninachukia kila njia ya uongo. PE.
na kwa sababu naona maagizo yako yote ni adili, nachukia kila njia potovu.
129 Sheria zako ni za ajabu, ndiyo sababu ninazitii.
Sheria zako ni za ajabu, hivyo ninazitii.
130 Ufafanuzi wa maneno yako huleta nuru; na kumpa ufahamu mjinga.
Kuingia kwa maneno yako kunaleta nuru, kunampa mjinga ufahamu.
131 Ninafungua kinywa changu na kutweta, maana ninazitamani amri zako.
Nimefungua kinywa changu na kuhema, nikitamani amri zako.
132 Unigeukie na unihurumie, kama ufanyavyo siku zote kwa wale walipendao jina lako.
Nigeukie na unihurumie, kama uwafanyiavyo siku zote wale wanaolipenda jina lako.
133 Uziongoze hatua zangu kwa neno lako; usiruhusu dhambi yeyote initawale.
Ongoza hatua zangu kulingana na neno lako, usiache dhambi yoyote initawale.
134 Unikomboe dhidi ya wanadamu waonevu ili niyatii maagizo yako.
Niokoe na uonevu wa wanadamu, ili niweze kutii mausia yako.
135 Uso wako umwangazie mtumishi wako, na unifundishe sheria zako.
Mwangazie mtumishi wako uso wako na unifundishe amri zako.
136 Mito ya machozi yatiririka kutoka machoni pangu kwa sababu watu hawaitii sheria yako. TSADHE.
Chemchemi za machozi zinatiririka kutoka machoni yangu, kwa kuwa sheria yako haifuatwi.
137 Wewe ni mwenye haki, Yahwe, na amri zako ni haki.
Ee Bwana, wewe ni mwenye haki, sheria zako ni sahihi.
138 Umezipa amri za agano lako haki na uaminifu.
Sheria ulizoziweka ni za haki, ni za kuaminika kikamilifu.
139 Hasira imeniangamiza kwa sababu adui zangu husahau maneno yako.
Jitihada yangu imenidhoofisha, kwa kuwa adui zangu wanayapuuza maneno yako.
140 Neno lako limepimwa sana, naye mtumishi wako analipenda.
Ahadi zako zimejaribiwa kikamilifu, mtumishi wako anazipenda.
141 Sina umuhimu na ninadharauliwa, lakini bado siyasahau maagizo yako.
Ingawa ni mdogo na ninadharauliwa, sisahau mausia yako.
142 Hukumu yako ni ya haki milele, na sheria yako ni ya kuaminika.
Haki yako ni ya milele, na sheria yako ni kweli.
143 Japo dhiki na taabu vimenipata, amri zako bado ni furaha yangu.
Shida na dhiki zimenipata, lakini amri zako ni furaha yangu.
144 Amri za agano lako ni za haki milele; unipe uelewa ili niweze kuishi. QOPH.
Sheria zako ni sahihi milele, hunipa ufahamu ili nipate kuishi.
145 Nililia kwa moyo wangu wote, “Unijibu, Yahwe, nitazishika sheria zako.
Ee Bwana, ninakuita kwa moyo wangu wote, nami nitayatii maagizo yako.
146 Ninakuita wewe; uniokoe, nami nitazitii amri za agano lako.”
Ninakuita; niokoe nami nitazishika sheria zako.
147 NInaamka asubuhi kabla jua halijachomoza na kulia kwa ajili ya msaada.
Ninaamka asubuhi na mapema na kukuomba msaada; nimeweka tumaini langu katika neno lako.
148 Ninatumaini katika maneno yako. Macho yangu yako wazi usiku kucha ili niweze kutafakari juu ya neno lako.
Sikufumba macho yangu usiku kucha, ili niweze kutafakari juu ya ahadi zako.
149 Sikia sauti yangu katika uaminifu wa agano lako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika amri zako za haki.
Usikie sauti yangu sawasawa na upendo wako, Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na sheria zako.
150 Wale wanaonitesa wananikaribia, lakini wako mbali na sheria yako.
Wale wanaopanga mipango miovu wako karibu nami, lakini wako mbali na sheria yako.
151 Wewe uko karibu, Yahwe, na amri zako ni za kuaminika.
Ee Bwana, hata hivyo wewe u karibu, na amri zako zote ni za kweli.
152 Muda mrefu uliopita nilijifunza kutoka katika amri za agano lako ulizoziweka katika mahali pa milele. RESH.
Tangu zamani nimejifunza kutoka shuhuda zako kwamba umezithibitisha ili zidumu milele.
153 Uyatazame mateso yangu na unisaidie, maana siisahau sheria yako.
Yaangalie mateso yangu, uniokoe, kwa kuwa sijasahau sheria yako.
154 Unitetee na kunikomboa; unihifadhi, kama ulivyo ahidi katika neno lako.
Nitetee katika hali hii yangu na unikomboe, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na ahadi yako.
155 Wokovu uko mbali na waovu, maana hawazipendi amri zako.
Wokovu uko mbali na waovu, kwa kuwa hawatafuti maagizo yako.
156 Matendo yako ya huruma ni makuu, Yahwe; uniweke hai; kama ufanyavyo siku zote.
Ee Bwana, huruma zako ni kuu, uyahifadhi maisha yangu sawasawa na sheria zako.
157 Watesi wangu na adui zangu ni wengi, lakini bado sijaenda mbali na amri za agano lako.
Adui wanaonitesa ni wengi, lakini mimi sitaziacha sheria zako.
158 Nimewaona wasaliti wakitia kinyaa kwa sababu hawalishiki neno lako.
Ninawatazama wasioamini kwa chuki, kwa kuwa hawalitii neno lako.
159 Tazama jinsi niyapendavyo maagizo yako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika uaminifu wa agano lako.
Tazama jinsi ninavyopenda mausia yako; Ee Bwana, uyahifadhi maisha yangu, sawasawa na upendo wako.
160 Kiini cha neno lako ni kweli; kila mmoja mwenye amri za haki hudumu milele. SHIN.
Maneno yako yote ni kweli, sheria zako zote za haki ni za milele.
161 Wakuu hunitesa bila sababu; moyo wangu hutetemeka, ukiogopa kutolitii neno lako.
Watawala wamenitesa bila sababu, lakini moyo wangu unatetemeka kwa neno lako.
162 Ninalifurahia neno lako kama apataye nyara nyingi.
Nafurahia ahadi zako kama mtu aliyepata mateka mengi.
163 Ninachukia na kudharau uongo, lakini naipenda sheria yako.
Ninachukia na kuchukizwa sana na uongo, lakini napenda sheria yako.
164 Mara saba kwa siku ninakusifu wewe kwa sababu ya amri zako za haki.
Ninakusifu mara saba kwa siku, kwa ajili ya sheria zako za haki.
165 Wana amani nyingi, waipendao sheria yako; hakuna cha kuwatia mashakani.
Wanaopenda sheria yako wana amani tele, wala hakuna kitu kinachoweza kuwakwaza.
166 Naungoja wokovu wako, Yahwe, na ninatii amri zako.
Ee Bwana, ninangojea wokovu wako, nami ninafuata amri zako,
167 Ninazishika amri zako thabiti, na ninazipenda sana.
Ninazitii sheria zako, kwa sababu ninazipenda mno.
168 Ninayashika maagizo yako na amri zako thabiti, kwa maana unajua kila kitu nifanyacho. TAV.
Nimetii mausia yako na sheria zako, kwa kuwa njia zangu zote zinajulikana kwako.
169 Sikia kilio changu, Yahwe; unipe uelewa wa neno lako.
Ee Bwana, kilio changu na kifike mbele zako, nipe ufahamu sawasawa na neno lako.
170 Maombi yangu yaje mbele zako; unisaidie, kama ulivyoahidi katika neno lako.
Maombi yangu na yafike mbele zako, niokoe sawasawa na ahadi yako.
171 Midomo yangu na imwage sifa, maana wewe unanifundisha sheria zako.
Midomo yangu na ibubujike sifa, kwa kuwa unanifundisha maagizo yako.
172 Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako, maana amri zako zote ni za haki.
Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako, kwa kuwa amri zako zote ni za haki.
173 Mkono wako unisaidie, maana nimechagua maagizo yako.
Mkono wako uwe tayari kunisaidia, kwa kuwa nimechagua mausia yako.
174 Ninautamani wokovu wako, Yahwe, na sheria yako ni furaha yangu.
Ee Bwana, ninatamani wokovu wako, na sheria yako ni furaha yangu.
175 Naomba niishi na nikusifu wewe, na amri zako za haki zinisaidie.
Nijalie kuishi ili nipate kukusifu, na sheria zako zinitegemeze.
176 Nimetanga-tanga kama kondoo aliyepotea; mtafute mtumishi wako, kwa maana sijazisahau amri zako.
Nimetangatanga kama kondoo aliyepotea. Mtafute mtumishi wako, kwa kuwa sijasahau amri zako.