< Zaburi 119 >
1 Wamebarikiwa wale ambao njia zao hazina lawama, waenendao katika sheria ya Yahwe.
行为完全、遵行耶和华律法的, 这人便为有福!
2 Wamebarikiwa wale wazishikao amri zake thabiti, wamtafutao kwa moyo wao wote.
遵守他的法度、一心寻求他的, 这人便为有福!
3 Hawatendi makosa; wanaenenda katika njia zake.
这人不做非义的事, 但遵行他的道。
4 Wewe umetuamuru kuyashika maagizo yako ili tuyachunguze kwa umakini.
耶和华啊,你曾将你的训词吩咐我们, 为要我们殷勤遵守。
5 Oh, ningependa njia zangu ziwe thabiti nizitii amri zako!
但愿我行事坚定, 得以遵守你的律例。
6 Ndipo sitaaibika nizifikiripo amri zako zote.
我看重你的一切命令, 就不至于羞愧。
7 Nitakushukuru wewe kwa unyofu wangu wa moyo nijifunzapo amri za haki yako.
我学了你公义的判语, 就要以正直的心称谢你。
8 Nitazitii amri zako; usiniache peke yangu. BETH.
我必守你的律例; 求你总不要丢弃我!
9 Ni jinsi gani kijana aweza kuendelea kuishi katika njia yake ya utakatifu? Ni kwa kulitii neno lako.
少年人用什么洁净他的行为呢? 是要遵行你的话!
10 Kwa moyo wangu wote ninakutafuta wewe; Usiniache nipotee mbali na maagizo yako.
我一心寻求了你; 求你不要叫我偏离你的命令。
11 Moyoni mwangu nimeliweka neno lako ili nisije nikakutenda dhambi.
我将你的话藏在心里, 免得我得罪你。
12 Umetukuka, Yahwe; unifundishe amri zako.
耶和华啊,你是应当称颂的! 求你将你的律例教训我!
13 Kwa kinywa changu nimetangaza amri ya haki yako yote ambayo umeifunua.
我用嘴唇传扬你口中的一切典章。
14 Ninafurahi katika njia ya amri za agano lako zaidi kuliko katika utajiri.
我喜悦你的法度, 如同喜悦一切的财物。
15 Nitayatafakari maagizo yako na kuzitilia maanani njia zako.
我要默想你的训词, 看重你的道路。
16 Ninafurahia katika amri zako; sitalisahau neno lako. GIMEL.
我要在你的律例中自乐; 我不忘记你的话。
17 Uwe mwema kwa mtumishi wako ili niweze kuishi na kulishika neno lako.
求你用厚恩待你的仆人,使我存活, 我就遵守你的话。
18 Ufungue macho yangu ili niweze kuona mambo ya ajabu katika sheria yako.
求你开我的眼睛, 使我看出你律法中的奇妙。
19 Mimi ni mgeni katika nchi; usizifiche amri zako mbali nami.
我是在地上作寄居的; 求你不要向我隐瞒你的命令!
20 Moyo wangu unauma kwa kutamani sana kuzijua amri zako za haki wakati wote.
我时常切慕你的典章, 甚至心碎。
21 Wewe huwakemea wenye kiburi, waliolaaniwa, wanao tanga-tanga mbali na amri zako.
受咒诅、偏离你命令的骄傲人, 你已经责备他们。
22 Uniokoe dhidi ya aibu na udhalilishaji, maana nimezitii amri za agano lako.
求你除掉我所受的羞辱和藐视, 因我遵守你的法度。
23 Ingawa watawala wanapanga njama na kunikashfu, mtumishi wako huzitafakali amri zako.
虽有首领坐着妄论我, 你仆人却思想你的律例。
24 Amri za agano lako ni furaha yangu, na washauri wangu. DALETH.
你的法度是我所喜乐的, 是我的谋士。
25 Uhai wangu unashikamana na mavumbi! nipe uhai kwa neno lako.
我的性命几乎归于尘土; 求你照你的话将我救活!
26 Nilikuambia mapito yangu, na ulinijibu; nifundishe sheria zako.
我述说我所行的,你应允了我; 求你将你的律例教训我!
27 Unifahamishe njia ya maagizo yako, ili niweze kutafakari juu ya mafundisho yako ya ajabu.
求你使我明白你的训词, 我就思想你的奇事。
28 Nimelemewa na huzuni! Nitie nguvu kwa neno lako.
我的心因愁苦而消化; 求你照你的话使我坚立!
29 Uiondoe kwangu njia ya udanganyifu; kwa wema wako unifundishe sheria yako.
求你使我离开奸诈的道, 开恩将你的律法赐给我!
30 Nimechagua njia ya uaminifu; siku zote nimeweka amri za haki yako mbele yangu.
我拣选了忠信的道, 将你的典章摆在我面前。
31 Ninashikamana na amri za agano lako; Yahwe, usiniache niaibike.
我持守你的法度; 耶和华啊,求你不要叫我羞愧!
32 Nitakimbia katika njia ya amri zako, kwa sababu wausukuma moyo wangu kufanya hivyo. HE
你开广我心的时候, 我就往你命令的道上直奔。
33 Unifundishe, Yahwe, njia za sheria yako, nami nitazishika hadi mwisho.
耶和华啊,求你将你的律例指教我, 我必遵守到底!
34 Unipe uelewa, nami nitazishika sheria zako; nitazitii kwa moyo wangu wote.
求你赐我悟性,我便遵守你的律法, 且要一心遵守。
35 Uniongoze katika njia ya amri zako, maana ninafurahi kuenenda katika hizo.
求你叫我遵行你的命令, 因为这是我所喜乐的。
36 Uelekeze moyo wangu kuzielekea amari za agano lako na uniweke mbali na matendo yasiyo haki tena.
求你使我的心趋向你的法度, 不趋向非义之财。
37 Uyageuze macho yangu dhidi ya kutazama mambo yasiyofaa; unihuishe katika njia zako.
求你叫我转眼不看虚假, 又叫我在你的道中生活。
38 Umtendee mtumishi wako ahadi ambayo uliifanya kwa wale wanaokuheshimu wewe.
你向敬畏你的人所应许的话, 求你向仆人坚定!
39 Uniondolee shutumu niiogopayo, maana hukumu zako za haki ni njema.
求你使我所怕的羞辱远离我, 因你的典章本为美。
40 Tazama, nimeyatamani maagizo yako; unihuishe katika haki yako. VAV.
我羡慕你的训词; 求你使我在你的公义上生活!
41 Ee Yahwe, unipe upendo wako usiokwisha na wokovu wako kulingana na ahadi yako;
耶和华啊,愿你照你的话,使你的慈爱, 就是你的救恩,临到我身上,
42 ndipo nitakuwa na jibu kwa ajili ya yule anayenidhihaki.
我就有话回答那羞辱我的, 因我倚靠你的话。
43 Usiliondoe neno la kweli mdomoni mwangu, maana nimesubiri kwa ajili ya amri zako za haki.
求你叫真理的话总不离开我口, 因我仰望你的典章。
44 Nitazitii sheria zako siku zote, milele na milele.
我要常守你的律法, 直到永永远远。
45 Nitaenenda salama, maana ninayatafuta maagizo yako.
我要自由而行, 因我素来考究你的训词。
46 Nitazinena amri zako thabiti mbele ya wafalme nami sitaaibika.
我也要在君王面前论说你的法度, 并不至于羞愧。
47 Ninafurahia katika amri zako, nizipendazo sana.
我要在你的命令中自乐; 这命令素来是我所爱的。
48 Nitaziinulia mikono yangu amri zako, nizipendazo; nitazitafakari sheria zako. ZAYIN.
我又要遵行你的命令, 这命令素来是我所爱的; 我也要思想你的律例。
49 Kumbuka ahadi yako kwa mtumishi wako kwa sababu umenipa tumaini.
求你记念向你仆人所应许的话, 叫我有盼望。
50 Hii ni faraja yangu katika mateso: kuwa ahadi yako imeniweka hai.
这话将我救活了; 我在患难中,因此得安慰。
51 Wenye kiburi wamenicheka, lakini sijaiacha sheria yako.
骄傲的人甚侮慢我, 我却未曾偏离你的律法。
52 Nimezitafakari amri zako za haki tangu zamani, Yahwe, nami ninajifariji mwenyewe.
耶和华啊,我记念你从古以来的典章, 就得了安慰。
53 Hasira kali imenishikilia kwa sababu ya waovu wanaoikataa sheria yako.
我见恶人离弃你的律法, 就怒气发作,犹如火烧。
54 Sheria zako zimekuwa nyimbo zangu katika nyumba ninayoishi kwa muda.
我在世寄居, 素来以你的律例为诗歌。
55 Ninalifikiria jina lako wakati wa usiku, Yahwe, na kuzishika sheria zako.
耶和华啊,我夜间记念你的名, 遵守你的律法。
56 Hili limekuwa zoezi langu kwa sababu nimeyatii maagizo yako. HETH.
我所以如此, 是因我守你的训词。
57 Yahwe ni sehemu yangu; nimeamua kuyatii maneno yake.
耶和华是我的福分; 我曾说,我要遵守你的言语。
58 Kwa bidii ninaomba neema yako kwa moyo wangu wote; unihurumie, kama neno lako lilivyo ahidi.
我一心求过你的恩; 愿你照你的话怜悯我!
59 Nilizichunguza njia zangu na kugeuzia miguu yangu kwenye amri za agano lako.
我思想我所行的道, 就转步归向你的法度。
60 Naharakisha na sichelewi kuzishika amri zako.
我急忙遵守你的命令, 并不迟延。
61 Kamba za waovu zimenifunga; nami sijaisahau sheria yako.
恶人的绳索缠绕我, 我却没有忘记你的律法。
62 Katikati ya usiku ninaamka kukushukuru wewe kwa sababu ya amri za haki yako.
我因你公义的典章, 半夜必起来称谢你。
63 Ninaurafiki na wale wanao kuabudu wewe, wale wote watiio maagizo yako.
凡敬畏你、守你训词的人, 我都与他作伴。
64 Yahwe, nchi, imejaa uaminifu wa agano lako; unifundishe sheria zako. TETH.
耶和华啊,你的慈爱遍满大地; 求你将你的律例教训我!
65 Wewe umemtendea mema mtumishi wako, Yahwe, sawasawa na neno lako.
耶和华啊,你向来是照你的话善待仆人。
66 Unifundishe utambuzi sahihi na uelewa, kwa kuwa nimeamini katika amri zako.
求你将精明和知识赐给我, 因我信了你的命令。
67 Kabla sijateswa nilipotea, lakini sasa nimelitii neno lako.
我未受苦以先走迷了路, 现在却遵守你的话。
68 Wewe ni mwema, na ndiye yule utendaye mema; unifundishe sheria zako.
你本为善,所行的也善; 求你将你的律例教训我!
69 Wenye kiburi wamenichafua kwa uongo, lakini niliyashika maagizo yako kwa moyo wangu wote.
骄傲人编造谎言攻击我, 我却要一心守你的训词。
70 Mioyo yao ni migumu, lakini ninafurahia katika sheria yako.
他们心蒙脂油, 我却喜爱你的律法。
71 Ni vizuri kwangu kuwa nimeteseka ili niweze kujifunza sheria zako.
我受苦是与我有益, 为要使我学习你的律例。
72 Maagizo yatokayo kinywani mwako ni ya thamani zaidi kwangu kuliko maelfu ya vipande vya dhahabu na fedha. YOD.
你口中的训言与我有益, 胜于千万的金银。
73 Mikono yako imeniumba na kunitengeneza; unipe uelewa ili niweze kujifunza amri zako.
你的手制造我,建立我; 求你赐我悟性,可以学习你的命令!
74 Wale wanao kucha wewe watafurahi wanionapo kwa sababu ninapata tumaini katika neno lako.
敬畏你的人见我就要欢喜, 因我仰望你的话。
75 Ninajua, Yahwe, kuwa amri zako ni za haki, na kuwa katika uaminifu ulinitesa.
耶和华啊,我知道你的判语是公义的; 你使我受苦是以诚实待我。
76 Agano lako aminifu na linifariji, kama ulivyomwahidi mtumishi wako.
求你照着应许仆人的话, 以慈爱安慰我。
77 Unihurumie ili niweze kuishi, kwa maana sheria yako ni furaha yangu.
愿你的慈悲临到我,使我存活, 因你的律法是我所喜爱的。
78 Wenye kiburi na waaibishwe, maana wamenitukana; bali mimi nitayatafakari maagizo yako.
愿骄傲人蒙羞,因为他们无理地倾覆我; 但我要思想你的训词。
79 Wale wote wanao kucha wewe na wanigeukie, wale wazijuao amri za agano lako.
愿敬畏你的人归向我, 他们就知道你的法度。
80 Moyo wangu uwe mkamilifu pamoja na heshima kwa sheria zako ili nisiaibike. KAPH.
愿我的心在你的律例上完全, 使我不致蒙羞。
81 Ninazimia kwa kutamani sana kuwa wewe unaweza kuniokoa! Ninamatumaini katika neno lako.
我心渴想你的救恩, 仰望你的应许。
82 Macho yangu yanatamani sana kuiona ahadi yako; ni lini utanifariji mimi?
我因盼望你的应许眼睛失明,说: 你何时安慰我?
83 Kwa maana nimekuwa kama kiriba katika moshi; sisahau sheria zako.
我好像烟薰的皮袋, 却不忘记你的律例。
84 Ni kwa muda gani gani mtumishi wako atalazimika kuyavumilia haya; ni lini utawahukumu wale wanaonitesa?
你仆人的年日有多少呢? 你几时向逼迫我的人施行审判呢?
85 Wenye kiburi wamenichimbia shimo, wasiotii sheria yako.
不从你律法的骄傲人为我掘了坑。
86 Amri zako zote ni za kuaminika; wale watu walinitesa bila ya haki; unisaidie.
你的命令尽都诚实; 他们无理地逼迫我,求你帮助我!
87 karibu kunifanya nifikie mwisho juu ya nchi hii, lakini siyakatai maagizo yako.
他们几乎把我从世上灭绝, 但我没有离弃你的训词。
88 Kwa upendo wako thabiti, uniweke hai, ili niweze kuzitii amri zako. LAMEDH.
求你照你的慈爱将我救活, 我就遵守你口中的法度。
89 Yahwe, neno lako linasimama milele; neno lako limefanywa imara mbinguni.
耶和华啊,你的话安定在天, 直到永远。
90 Uaminifu wako wadumu kwa ajili ya vizazi vyote; umeiimarisha nchi, nayo inadumu.
你的诚实存到万代; 你坚定了地,地就长存。
91 Vitu yote yaliendelea mpaka leo hii, kama vile ulivyosema katika amri zako za haki, maana vitu vyote ni watumishi wako.
天地照你的安排存到今日; 万物都是你的仆役。
92 Kama sheria yako isingekuwa furaha yangu, ningeangamia katika mateso yangu.
我若不是喜爱你的律法, 早就在苦难中灭绝了!
93 Sitayasahau kamwe maagizo yako, maana kupitia hayo umeniweka hai.
我永不忘记你的训词, 因你用这训词将我救活了。
94 Mimi ni wako, kwa maana ninayatafuta maagizo yao.
我是属你的,求你救我, 因我寻求了你的训词。
95 Waovu hujiandaa kuniangamiza, lakini nitatafuta kuzielewa amri za agano lako.
恶人等待我,要灭绝我, 我却要揣摩你的法度。
96 Nimeona kuwa kila kitu kina mipaka, lakini amri zako ni pana, zaidi ya mipaka. MEM.
我看万事尽都有限, 惟有你的命令极其宽广。
97 Oh ni jinsi gani naipenda sheria yako! Ni tafakari yangu mchana kutwa.
我何等爱慕你的律法, 终日不住地思想。
98 Amri zako hunifanya mwenye hekima kuliko adui zangu, maana amri zako siku zote ziko pamoja nami.
你的命令常存在我心里, 使我比仇敌有智慧。
99 Ninauelewa zaidi kuliko walimu wangu wote, kwa maana ninazitafakari amri za agano lako.
我比我的师傅更通达, 因我思想你的法度。
100 Ninaelewa kuliko wale wanaonizidi umri; hii ni kwa sababu nimeyashika maagizo yako.
我比年老的更明白, 因我守了你的训词。
101 Nimeiepusha miguu yangu na kila njia ya uovu ili niweze kulitii neno lako.
我禁止我脚走一切的邪路, 为要遵守你的话。
102 Sijaenda kinyume na amri zako za haki, kwa maana wewe umenifundisha.
我没有偏离你的典章, 因为你教训了我。
103 Ni jinsi gani maneno yako ni matamu kwenye majaribu yangu, naam, matamu kuliko asali kinywani mwangu!
你的言语在我上膛何等甘美, 在我口中比蜜更甜!
104 Kupitia maagizo yako ninapata utambuzi; kwa hiyo kila njia isiyo ya kweli.
我借着你的训词得以明白, 所以我恨一切的假道。
105 Neno lako ni taa ya mguu miguu yangu na mwanga wa njia yangu.
你的话是我脚前的灯, 是我路上的光。
106 Nimeapa na nimethibitisha, kuwa nitazitii amri za haki yako.
你公义的典章,我曾起誓遵守, 我必按誓而行。
107 Nimeteswa sana; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika neno lako.
我甚是受苦; 耶和华啊,求你照你的话将我救活!
108 Yahwe, tafadhali pokea dhabihu yangu ya hiari ya kinywa changu, na unifundishe amri zako za haki.
耶和华啊,求你悦纳我口中的赞美为供物, 又将你的典章教训我!
109 Uhai wangu ziku zote uko mkononi mwangu, lakini bado sisahau sheria yako.
我的性命常在危险之中, 我却不忘记你的律法。
110 Waovu wamenitegea mtego, lakini sijapotea mbali na maagizo yako.
恶人为我设下网罗, 我却没有偏离你的训词。
111 Nimezifanya amri za agano lako kama urithi wangu milele, maana hizo ni furaha ya moyo wangu.
我以你的法度为永远的产业, 因这是我心中所喜爱的。
112 Moyo wangu umewekwa kuzitii sheria zako milele mpaka mwisho kabisa. SAMEKH.
我的心专向你的律例, 永远遵行,一直到底。
113 Ninawachukia watu wa kusita-sita, lakini naipenda sheria yako.
心怀二意的人为我所恨; 但你的律法为我所爱。
114 Wewe ni ficho langu na ngao yangu; nalingoja neno lako.
你是我藏身之处,又是我的盾牌; 我甚仰望你的话语。
115 Ondokeni kwangu, ninyi mtendao uovu, ili niweze kuzitii amri za Mungu wangu.
作恶的人哪,你们离开我吧! 我好遵守我 神的命令。
116 Uniwezeshe kwa neno lako ili niweze kuishi na nisiaibike na matumaini yangu.
求你照你的话扶持我,使我存活, 也不叫我因失望而害羞。
117 Unisaidie, nami nitakuwa salama; siki zote nitazitafakari sheria zako.
求你扶持我,我便得救, 时常看重你的律例。
118 Wewe huwakataa wale wote wapoteao mbali na sheria zako, maana watu hao ni wadanganyifu na si wakuaminika.
凡偏离你律例的人,你都轻弃他们, 因为他们的诡诈必归虚空。
119 Wewe huwaondoa waovu wa nchi kama takataka; kwa hiyo ninazipenda amri zako thabiti.
凡地上的恶人,你除掉他,好像除掉渣滓; 因此我爱你的法度。
120 Mwili wangu hutetemeka kwa hofu yako, na ninaziogopa amri za haki yako. AYIN.
我因惧怕你,肉就发抖; 我也怕你的判语。
121 Ninafanya kilicho sahihi na haki; usiniache kwa watesi wangu.
我行过公平和公义, 求你不要撇下我给欺压我的人!
122 Uwe mdhamini wa ustawi wa mtumishi wako; usiwaache wenye kiburi wanionee.
求你为仆人作保,使我得好处, 不容骄傲人欺压我!
123 Macho yangu yanachoka kwa kuusubiri wokovu wako na neno lako la haki.
我因盼望你的救恩 和你公义的话眼睛失明。
124 Mwoneshe mtumishi wako uaminifu wa agano lako, na unifundishe sheria zako.
求你照你的慈爱待仆人, 将你的律例教训我。
125 Mimi ni mtumishi wako; unipe uelewa ili niweze kuzijua amri za agano lako.
我是你的仆人,求你赐我悟性, 使我得知你的法度。
126 Ni wakati wa Yahwe kutenda, kwa maana watu wamevunja sheria yako.
这是耶和华降罚的时候, 因人废了你的律法。
127 Hakika ninazipenda amri zako kuliko dhahabu, naam, kuliko dhahabu safi.
所以,我爱你的命令胜于金子, 更胜于精金。
128 Hivyo ninayafuata maagizo yako yote kwa makini, na ninachukia kila njia ya uongo. PE.
你一切的训词,在万事上我都以为正直; 我却恨恶一切假道。
129 Sheria zako ni za ajabu, ndiyo sababu ninazitii.
你的法度奇妙, 所以我一心谨守。
130 Ufafanuzi wa maneno yako huleta nuru; na kumpa ufahamu mjinga.
你的言语一解开就发出亮光, 使愚人通达。
131 Ninafungua kinywa changu na kutweta, maana ninazitamani amri zako.
我张口而气喘, 因我切慕你的命令。
132 Unigeukie na unihurumie, kama ufanyavyo siku zote kwa wale walipendao jina lako.
求你转向我,怜悯我, 好像你素常待那些爱你名的人。
133 Uziongoze hatua zangu kwa neno lako; usiruhusu dhambi yeyote initawale.
求你用你的话使我脚步稳当, 不许什么罪孽辖制我。
134 Unikomboe dhidi ya wanadamu waonevu ili niyatii maagizo yako.
求你救我脱离人的欺压, 我要遵守你的训词。
135 Uso wako umwangazie mtumishi wako, na unifundishe sheria zako.
求你用脸光照仆人, 又将你的律例教训我。
136 Mito ya machozi yatiririka kutoka machoni pangu kwa sababu watu hawaitii sheria yako. TSADHE.
我的眼泪下流成河, 因为他们不守你的律法。
137 Wewe ni mwenye haki, Yahwe, na amri zako ni haki.
耶和华啊,你是公义的; 你的判语也是正直的!
138 Umezipa amri za agano lako haki na uaminifu.
你所命定的法度是凭公义和至诚。
139 Hasira imeniangamiza kwa sababu adui zangu husahau maneno yako.
我心焦急,如同火烧, 因我敌人忘记你的言语。
140 Neno lako limepimwa sana, naye mtumishi wako analipenda.
你的话极其精炼, 所以你的仆人喜爱。
141 Sina umuhimu na ninadharauliwa, lakini bado siyasahau maagizo yako.
我微小,被人藐视, 却不忘记你的训词。
142 Hukumu yako ni ya haki milele, na sheria yako ni ya kuaminika.
你的公义永远长存; 你的律法尽都真实。
143 Japo dhiki na taabu vimenipata, amri zako bado ni furaha yangu.
我遭遇患难愁苦, 你的命令却是我所喜爱的。
144 Amri za agano lako ni za haki milele; unipe uelewa ili niweze kuishi. QOPH.
你的法度永远是公义的; 求你赐我悟性,我就活了。
145 Nililia kwa moyo wangu wote, “Unijibu, Yahwe, nitazishika sheria zako.
耶和华啊,我一心呼吁你; 求你应允我,我必谨守你的律例!
146 Ninakuita wewe; uniokoe, nami nitazitii amri za agano lako.”
我向你呼吁,求你救我! 我要遵守你的法度。
147 NInaamka asubuhi kabla jua halijachomoza na kulia kwa ajili ya msaada.
我趁天未亮呼求; 我仰望了你的言语。
148 Ninatumaini katika maneno yako. Macho yangu yako wazi usiku kucha ili niweze kutafakari juu ya neno lako.
我趁夜更未换将眼睁开, 为要思想你的话语。
149 Sikia sauti yangu katika uaminifu wa agano lako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika amri zako za haki.
求你照你的慈爱听我的声音; 耶和华啊,求你照你的典章将我救活!
150 Wale wanaonitesa wananikaribia, lakini wako mbali na sheria yako.
追求奸恶的人临近了; 他们远离你的律法。
151 Wewe uko karibu, Yahwe, na amri zako ni za kuaminika.
耶和华啊,你与我相近; 你一切的命令尽都真实!
152 Muda mrefu uliopita nilijifunza kutoka katika amri za agano lako ulizoziweka katika mahali pa milele. RESH.
我因学你的法度, 久已知道是你永远立定的。
153 Uyatazame mateso yangu na unisaidie, maana siisahau sheria yako.
求你看顾我的苦难,搭救我, 因我不忘记你的律法。
154 Unitetee na kunikomboa; unihifadhi, kama ulivyo ahidi katika neno lako.
求你为我辨屈,救赎我, 照你的话将我救活。
155 Wokovu uko mbali na waovu, maana hawazipendi amri zako.
救恩远离恶人, 因为他们不寻求你的律例。
156 Matendo yako ya huruma ni makuu, Yahwe; uniweke hai; kama ufanyavyo siku zote.
耶和华啊,你的慈悲本为大; 求你照你的典章将我救活。
157 Watesi wangu na adui zangu ni wengi, lakini bado sijaenda mbali na amri za agano lako.
逼迫我的,抵挡我的,很多, 我却没有偏离你的法度。
158 Nimewaona wasaliti wakitia kinyaa kwa sababu hawalishiki neno lako.
我看见奸恶的人就甚憎恶, 因为他们不遵守你的话。
159 Tazama jinsi niyapendavyo maagizo yako; uniweke hai, Yahwe, kama ulivyoahidi katika uaminifu wa agano lako.
你看我怎样爱你的训词! 耶和华啊,求你照你的慈爱将我救活!
160 Kiini cha neno lako ni kweli; kila mmoja mwenye amri za haki hudumu milele. SHIN.
你话的总纲是真实; 你一切公义的典章是永远长存。
161 Wakuu hunitesa bila sababu; moyo wangu hutetemeka, ukiogopa kutolitii neno lako.
首领无故地逼迫我, 但我的心畏惧你的言语。
162 Ninalifurahia neno lako kama apataye nyara nyingi.
我喜爱你的话, 好像人得了许多掳物。
163 Ninachukia na kudharau uongo, lakini naipenda sheria yako.
谎话是我所恨恶所憎嫌的; 惟你的律法是我所爱的。
164 Mara saba kwa siku ninakusifu wewe kwa sababu ya amri zako za haki.
我因你公义的典章一天七次赞美你。
165 Wana amani nyingi, waipendao sheria yako; hakuna cha kuwatia mashakani.
爱你律法的人有大平安, 什么都不能使他们绊脚。
166 Naungoja wokovu wako, Yahwe, na ninatii amri zako.
耶和华啊,我仰望了你的救恩, 遵行了你的命令。
167 Ninazishika amri zako thabiti, na ninazipenda sana.
我心里守了你的法度; 这法度我甚喜爱。
168 Ninayashika maagizo yako na amri zako thabiti, kwa maana unajua kila kitu nifanyacho. TAV.
我遵守了你的训词和法度, 因我一切所行的都在你面前。
169 Sikia kilio changu, Yahwe; unipe uelewa wa neno lako.
耶和华啊,愿我的呼吁达到你面前, 照你的话赐我悟性。
170 Maombi yangu yaje mbele zako; unisaidie, kama ulivyoahidi katika neno lako.
愿我的恳求达到你面前, 照你的话搭救我。
171 Midomo yangu na imwage sifa, maana wewe unanifundisha sheria zako.
愿我的嘴发出赞美的话, 因为你将律例教训我。
172 Ulimi wangu na uimbe kuhusu neno lako, maana amri zako zote ni za haki.
愿我的舌头歌唱你的话, 因你一切的命令尽都公义。
173 Mkono wako unisaidie, maana nimechagua maagizo yako.
愿你用手帮助我, 因我拣选了你的训词。
174 Ninautamani wokovu wako, Yahwe, na sheria yako ni furaha yangu.
耶和华啊,我切慕你的救恩! 你的律法也是我所喜爱的。
175 Naomba niishi na nikusifu wewe, na amri zako za haki zinisaidie.
愿我的性命存活,得以赞美你! 愿你的典章帮助我!
176 Nimetanga-tanga kama kondoo aliyepotea; mtafute mtumishi wako, kwa maana sijazisahau amri zako.
我如亡羊走迷了路,求你寻找仆人, 因我不忘记你的命令。