< Zaburi 116 >

1 Nampenda Yahwe kwa kuwa anasikia sauti yangu na kuomba kwangu kwa ajili ya huruma.
Amo a Yavé, Porque escucha mi voz y mis súplicas,
2 Kwa sababu alinisikiliza, nitamuita yeye ningali ninaishi.
Porque inclina a mí su oído. Por tanto, [lo] invocaré mientras viva.
3 Kamba za mauti zilinizunguka, na mitego ya kuzimu ilinikabili; niliona dhiki na huzuni. (Sheol h7585)
Me rodearon las ataduras de la muerte. Me cayeron los terrores del Seol. Hallé angustia y tristeza. (Sheol h7585)
4 Kisha niliita kwa jina la Yahwe: “Tafadhali Yahwe, uiokoe nafsi yangu.”
Entonces invoqué el Nombre de Yavé: Oh Yavé, te busco, libra mi alma.
5 Yahwe ni mwenye neema na haki; Mungu wetu ni mwenye huruma.
Bondadoso y justo es Yavé. Sí, misericordioso es nuestro ʼElohim.
6 Yahwe huwalinda wasio na hila; nilishushwa chini akaniokoa.
Yavé guarda a los sencillos. Estaba yo postrado Y Él me salvó.
7 Nafsi yangu inaweza kurudi mahali pake pa kupumzika, kwa kuwa Yahwe amekuwa mwema kwangu.
Vuelve, alma mía, a tu reposo, Porque Yavé te llenó de bien.
8 Kwa maana uliokoa uhai wangu dhidi ya kifo, mcho yangu dhidi ya machozi, na miguu yangu dhidi ya kujikwaa.
Tú libraste mi vida de la muerte, Mis ojos, de las lágrimas, Y mis pies, de tropezar.
9 Nitamtumikia Yahwe katika nchi ya walio hai.
Andaré delante de Yavé En la tierra de los vivientes.
10 Nilimwamini yeye, hata niliposema, “nimeteswa sana.”
Creí, por tanto hablé: Estoy afligido en gran manera.
11 Kwa haraka nilisema, “Watu wote ni waongo.”
Y dije en mi apresuramiento: Todo hombre es mentiroso.
12 Nimlipeje Yahwe kwa wema wake wote kwangu?
¿Qué pagaré a Yavé Por todos sus beneficios para mí?
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu, na kuliitia jina la Yahwe.
Levantaré la copa de la salvación E invocaré el Nombre de Yavé.
14 Nitatimiza viapo vyangu kwa Yahwe katika uwepo wa watu wake wote.
A Yavé cumpliré mis votos En presencia de todo su pueblo.
15 Mauti ya wacha Mungu ina thamani machoni pa Mungu.
Estimada es a los ojos de Yavé La muerte de sus santos.
16 Ee Yahwe, hakika, mimi ni mtumishi wako; mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umefungua vifungo vyangu.
Oh Yavé, ciertamente yo soy tu esclavo. Esclavo tuyo soy, hijo de tu esclava, Tú desataste mis ataduras.
17 Nitakutolea dhabihu ya shukrani na nitaliitia jina la Yahwe.
Te ofreceré sacrificio de acción de gracias E invocaré el Nombre de Yavé.
18 Nitatimiza viapo vyangu kwa Yahwe katika uwepo wa watu wake wote,
A Yavé cumpliré mis votos, En presencia de todo su pueblo,
19 katika nyua za nyumba ya Yahwe, katikati yako, Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
En los patios de la Casa de Yavé, En medio de [ti], oh Jerusalén. ¡Aleluya!

< Zaburi 116 >