< Zaburi 116 >

1 Nampenda Yahwe kwa kuwa anasikia sauti yangu na kuomba kwangu kwa ajili ya huruma.
אהבתי כי ישמע יהוה את קולי תחנוני׃
2 Kwa sababu alinisikiliza, nitamuita yeye ningali ninaishi.
כי הטה אזנו לי ובימי אקרא׃
3 Kamba za mauti zilinizunguka, na mitego ya kuzimu ilinikabili; niliona dhiki na huzuni. (Sheol h7585)
אפפוני חבלי מות ומצרי שאול מצאוני צרה ויגון אמצא׃ (Sheol h7585)
4 Kisha niliita kwa jina la Yahwe: “Tafadhali Yahwe, uiokoe nafsi yangu.”
ובשם יהוה אקרא אנה יהוה מלטה נפשי׃
5 Yahwe ni mwenye neema na haki; Mungu wetu ni mwenye huruma.
חנון יהוה וצדיק ואלהינו מרחם׃
6 Yahwe huwalinda wasio na hila; nilishushwa chini akaniokoa.
שמר פתאים יהוה דלותי ולי יהושיע׃
7 Nafsi yangu inaweza kurudi mahali pake pa kupumzika, kwa kuwa Yahwe amekuwa mwema kwangu.
שובי נפשי למנוחיכי כי יהוה גמל עליכי׃
8 Kwa maana uliokoa uhai wangu dhidi ya kifo, mcho yangu dhidi ya machozi, na miguu yangu dhidi ya kujikwaa.
כי חלצת נפשי ממות את עיני מן דמעה את רגלי מדחי׃
9 Nitamtumikia Yahwe katika nchi ya walio hai.
אתהלך לפני יהוה בארצות החיים׃
10 Nilimwamini yeye, hata niliposema, “nimeteswa sana.”
האמנתי כי אדבר אני עניתי מאד׃
11 Kwa haraka nilisema, “Watu wote ni waongo.”
אני אמרתי בחפזי כל האדם כזב׃
12 Nimlipeje Yahwe kwa wema wake wote kwangu?
מה אשיב ליהוה כל תגמולוהי עלי׃
13 Nitakiinua kikombe cha wokovu, na kuliitia jina la Yahwe.
כוס ישועות אשא ובשם יהוה אקרא׃
14 Nitatimiza viapo vyangu kwa Yahwe katika uwepo wa watu wake wote.
נדרי ליהוה אשלם נגדה נא לכל עמו׃
15 Mauti ya wacha Mungu ina thamani machoni pa Mungu.
יקר בעיני יהוה המותה לחסידיו׃
16 Ee Yahwe, hakika, mimi ni mtumishi wako; mimi ni mtumishi wako, mwana wa mjakazi wako; umefungua vifungo vyangu.
אנה יהוה כי אני עבדך אני עבדך בן אמתך פתחת למוסרי׃
17 Nitakutolea dhabihu ya shukrani na nitaliitia jina la Yahwe.
לך אזבח זבח תודה ובשם יהוה אקרא׃
18 Nitatimiza viapo vyangu kwa Yahwe katika uwepo wa watu wake wote,
נדרי ליהוה אשלם נגדה נא לכל עמו׃
19 katika nyua za nyumba ya Yahwe, katikati yako, Yerusalemu. Msifuni Yahwe.
בחצרות בית יהוה בתוככי ירושלם הללו יה׃

< Zaburi 116 >