< Zaburi 115 >

1 Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
Nicht uns, HERR, nicht uns, sondern deinem Namen gib Ehre um deine Gnade und Wahrheit!
2 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
Warum sollen die Heiden sagen: Wo ist nun ihr Gott?
3 Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
Aber unser Gott ist im Himmel; er kann schaffen, was er will.
4 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Jener Götzen aber sind Silber und Gold, von Menschenhänden gemacht.
5 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
Sie haben Mäuler und reden nicht; sie haben Augen und sehen nicht;
6 zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
sie haben Ohren und hören nicht; sie haben Nasen und riechen nicht;
7 Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
sie haben Hände und greifen nicht; Füße haben sie und gehen nicht und reden nicht durch ihren Hals.
8 Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
Die solche machen, sind gleich also, und alle, die auf sie hoffen.
9 Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
Aber Israel hoffe auf den HERRN; der ist ihre Hilfe und Schild.
10 Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
Das Haus Aaron hoffe auf den HERRN; der ist ihre Hilfe und Schild.
11 Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
Die den HERRN fürchten, hoffen auch auf den HERRN; der ist ihre Hilfe und Schild.
12 Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
Der HERR denket an uns und segnet uns. Er segnet das Haus Israel; er segnet das Haus Aaron;
13 Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
er segnet, die den HERRN fürchten, beide Kleine und Große.
14 Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
Der HERR segne euch je mehr und mehr, euch und eure Kinder!
15 Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
Ihr seid die Gesegneten des HERRN, der Himmel und Erde gemacht hat.
16 Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
Der Himmel allenthalben ist des HERRN; aber die Erde hat er den Menschenkindern gegeben.
17 Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
Die Toten werden dich, HERR, nicht loben, noch die hinunterfahren in die Stille,
18 bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.
sondern wir loben den HERRN von nun an bis in Ewigkeit. Halleluja!

< Zaburi 115 >