< Zaburi 115 >

1 Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
Nicht uns, Jahwe, nicht uns, sondern deinem Namen gieb Ehre, um deiner Gnade, um deiner Treue willen!
2 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
Warum sollen die Heiden sagen: “Wo ist doch ihr Gott?”
3 Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
Ist doch unser Gott im Himmel: alles, was ihm beliebte, hat er gethan.
4 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Ihre Götzen sind Silber und Gold, ein Werk von Menschenhänden.
5 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
Sie haben einen Mund und reden nicht; sie haben Augen und sehen nicht.
6 zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
Sie haben Ohren und hören nicht; sie haben eine Nase und riechen nicht.
7 Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
Hände haben sie und tasten nicht, Füße haben sie und gehen nicht; sie sprechen nicht mit ihrer Kehle.
8 Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
Ihnen gleich werden die, die sie verfertigen, jeder, der auf sie vertraut.
9 Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
Israel, vertraue auf Jahwe - er ist ihre Hilfe und ihr Schild!
10 Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
Ihr vom Hause Aarons, vertraut auf Jahwe - er ist ihre Hilfe und ihr Schild!
11 Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
Die ihr Jahwe fürchtet, vertraut auf Jahwe - er ist ihre Hilfe und ihr Schild!
12 Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
Jahwe hat unser gedacht: er wird segnen, wird segnen das Haus Israel, segnen das Haus Aarons.
13 Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
Er wird segnen, die Jahwe fürchten, die Kleinen samt den Großen.
14 Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
Jahwe wolle zu euch hinzuthun, zu euch und zu euren Kindern.
15 Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
Gesegnet seid ihr von Jahwe, der Himmel und Erde gemacht hat.
16 Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
Der Himmel ist Himmel Jahwes, aber die Erde hat er den Menschen gegeben.
17 Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
Nicht die Toten rühmen Jahwe, noch einer von denen, die in die Stille hinabgefahren:
18 bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.
aber wir preisen Jah, von nun an bis in Ewigkeit. Rühmet Jah!

< Zaburi 115 >