< Zaburi 115 >
1 Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
Pas à nous, Yahvé, pas à nous, mais que ton nom soit glorifié, pour ta bonté et pour l'amour de ta vérité.
2 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
Pourquoi les nations diraient-elles, « Où est leur Dieu, maintenant? »
3 Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
Mais notre Dieu est dans les cieux. Il fait ce qui lui plaît.
4 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Leurs idoles sont l'argent et l'or, le travail de la main de l'homme.
5 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
Ils ont une bouche, mais ils ne parlent pas. Ils ont des yeux, mais ils ne voient pas.
6 zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
Ils ont des oreilles, mais ils n'entendent pas. Ils ont un nez, mais ils ne sentent pas.
7 Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
Ils ont des mains, mais ils ne sentent pas. Ils ont des pieds, mais ils ne marchent pas, ils ne parlent pas non plus par la gorge.
8 Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
Ceux qui les font seront comme eux; oui, tous ceux qui ont confiance en eux.
9 Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
Israël, aie confiance en Yahvé! Il est leur aide et leur bouclier.
10 Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
Maison d'Aaron, ayez confiance en Yahvé! Il est leur aide et leur bouclier.
11 Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
Vous qui craignez Yahvé, ayez confiance en Yahvé! Il est leur aide et leur bouclier.
12 Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
Yahvé se souvient de nous. Il nous bénira. Il bénira la maison d'Israël. Il bénira la maison d'Aaron.
13 Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
Il bénira ceux qui craignent Yahvé, à la fois petites et grandes.
14 Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
Que Yahvé vous augmente de plus en plus, vous et vos enfants.
15 Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
Vous êtes bénis par Yahvé, qui a fait le ciel et la terre.
16 Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
Les cieux sont les cieux de l'Éternel, mais il a donné la terre aux enfants des hommes.
17 Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
Les morts ne louent pas Yahvé, ni ceux qui descendent dans le silence,
18 bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.
mais nous bénirons Yah, à partir de maintenant et pour toujours. Louez Yah!