< Zaburi 115 >

1 Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
Not unto us, O Yahweh, not unto us, —but, unto thine own Name, give glory, concerning thy lovingkindness, concerning thy faithfulness.
2 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
Wherefore should the nations say, Pray where is their God?
3 Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
When, our God, is in the heavens, Whatsoever he pleased, hath he done.
4 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Their idols, are silver and gold, the works of the hands of men, —
5 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
A mouth, have they, but they speak not, Eyes, have they, but they see not;
6 zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
Ears, have they, but they hear not, A nose, have they, but they smell not:
7 Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
Their hands! but they feel not Their feet! but they walk not, No sound make they in their throat.
8 Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
Like unto them, shall be they who make them, Every one who trusteth in them.
9 Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
O Israel! trust thou in Yahweh, Their help and their shield, is he!
10 Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
O house of Aaron! trust ye in Yahweh, Their help and their shield, is he!
11 Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
Ye that revere Yahweh! trust in Yahweh, Their help and their shield, is he!
12 Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
Yahweh, hath remembered us, he will bless—He will bless the house of Israel, He will bless the house of Aaron;
13 Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
He will bless them who revere Yahweh, the small with the great.
14 Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
Yahweh multiply you, You, and your children.
15 Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
Blessed are ye of Yahweh, who made the heavens and the earth:
16 Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
As for the heavens, the heavens, belong to Yahweh, but the earth, hath he given to the sons of men.
17 Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
The dead, cannot praise Yah, nor any that go down into silence;
18 bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.
But, we, will bless Yah, from henceforth even unto times age-abiding. Praise ye Yah.

< Zaburi 115 >