< Zaburi 115 >
1 Sio kwetu, Yahwe, sio kwetu, bali kwa jina lako ulete heshima, kwa ajili ya uaminifu wa agano lako na uaminifu wako.
Not unto us, O LORD! not unto us, But unto thy name, give glory, For thy mercy and thy truth's sake!
2 Kwa nini mataifa yalazimike kusema, “Yuko wapi Mungu wako?”
Why should the nations say, “Where is now their God?”
3 Mungu wetu aliye mbinguni; hufanya chochote apendacho.
Our God is in the heavens; He doeth whatever he pleaseth.
4 Sanamu za mataifa ni fedha na dhahabu, kazi ya mikono ya wanadamu.
Their idols are silver and gold, The work of men's hands:
5 Sanamu hizo zina vinywa, lakini haziongei; zina macho, lakini hazioni;
They have mouths, but they speak not; Eyes have they, but they see not;
6 zina masikio, lakini hazisikii; zina pua lakini hazinusi.
They have ears, but they hear not; Noses have they, but they smell not;
7 Sanamu hizo zina mikono, lakini hazishiki; zina miguu, lakini haziwezi kutembea; wala haziongei kutoka viywani mwao.
They have hands, but they handle not; They have feet, but they walk not; Nor do they speak with their throats.
8 Wale wanao zitengeneza wanafanana nazo, vile vile yeyote anaye amini katika hizo.
They who make them are like unto them; And so is every one that trusteth in them.
9 Israeli, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
O Israel! trust thou in the LORD! He is their help and their shield.
10 Nyumba ya Haruni, amini katika Yahwe; yeye ni msaada wako na ngao yako.
O house of Aaron! trust ye in the LORD! He is their help and their shield.
11 Ninyi mnao mheshumu Yahwe, mwamini yeye; yeye ni msaada wenu na ngao yenu.
Ye that fear the LORD trust in the LORD! He is their help and their shield.
12 Yahwe hutukumbuka sisi na atatubariki; ataibariki familia ya Israeli; atabariki familia ya Haruni.
The LORD hath been mindful of us; he will bless us; He will bless the house of Israel; He will bless the house of Aaron.
13 Atawabariki wale wanao muheshimu yeye, wote vijana na wazee.
He will bless them that fear the LORD, both small and great.
14 Yahwe na awaongeze ninyi zaidi na zaidi, ninyi pamoja na watoto wenu.
The LORD will increase you more and more, You and your children.
15 Yahwe na awabariki, aliyeziumba mbingu na nchi.
Blessed are ye of the LORD, Who made heaven and earth.
16 Mbingu ni za Yahwe; lakini nchi amewapa wanadamu.
The heaven is the LORD'S heaven; But the earth he hath given to the sons of men.
17 Wafu hawamsifu Yahwe, wala wote washukao chini kwenye ukimya;
The dead praise not the LORD, —No one who goeth down into silence.
18 bali tutamtukuza Yahwe sasa na hata milele. Msifuni Yahwe.
But we will bless the LORD, From this time forth even for ever! Praise ye the LORD!